< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Притчи Соломона. Сын мудрый радует отца, а сын глупый - огорчение для его матери.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Не доставляют пользы сокровища неправедные, правда же избавляет от смерти.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Не допустит Господь терпеть голод душе праведного, стяжание же нечестивых исторгнет.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Ленивая рука делает бедным, а рука прилежных обогащает.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Собирающий во время лета - сын разумный, спящий же во время жатвы - сын беспутный.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Благословения - на голове праведника, уста же беззаконных заградит насилие.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
Память праведника пребудет благословенна, а имя нечестивых омерзеет.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Мудрый сердцем принимает заповеди, а глупый устами преткнется.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Кто ходит в непорочности, тот ходит безопасно; а кто превращает пути свои, тот будет наказан.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Кто мигает глазами, тот причиняет досаду, а глупый устами преткнется.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Уста праведника - источник жизни, уста же беззаконных заградит насилие.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Ненависть возбуждает раздоры, но любовь покрывает все грехи.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
В устах разумного находится мудрость, но на теле глупого - розга.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Мудрые сберегают знание, но уста глупого близкая погибель.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
Имущество богатого - крепкий город его, беда для бедных - скудость их.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Труды праведного - к жизни, успех нечестивого - ко греху.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Кто хранит наставление, тот на пути к жизни; а отвергающий обличение - блуждает.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Кто скрывает ненависть, у того уста лживые; и кто разглашает клевету, тот глуп.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
При многословии не миновать греха, а сдерживающий уста свои - разумен.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
Отборное серебро язык праведного, сердце же нечестивых - ничтожество.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Уста праведного пасут многих, а глупые умирают от недостатка разума.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
Благословение Господне - оно обогащает и печали с собою не приносит.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Для глупого преступное деяние как бы забава, а человеку разумному свойственна мудрость.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Чего страшится нечестивый, то и постигнет его, а желание праведников исполнится.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Как проносится вихрь, так нет более нечестивого; а праведник - на вечном основании.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Что уксус для зубов и дым для глаз, то ленивый для посылающих его.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
Страх Господень прибавляет дней, лета же нечестивых сократятся.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
Ожидание праведников радость, а надежда нечестивых погибнет.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
Путь Господень - твердыня для непорочного и страх для делающих беззаконие.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Праведник во веки не поколеблется, нечестивые же не поживут на земле.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
Уста праведника источают мудрость, а язык зловредный отсечëтся.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Уста праведного знают благоприятное, а уста нечестивых - развращенное.

< Mithali 10 >