< Mithali 10 >
1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Provérbios de Salomão. O filho sábio alegra a seu pai, mas o filho louco é a tristeza de sua mãe.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Os tesouros da impiedade de nada aproveitam; porém a justiça livra da morte.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
O Senhor não deixa ter fome a alma do justo, mas a fazenda dos ímpios rechaça.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
O que trabalha com mão enganosa empobrece, mas a mão dos diligentes enriquece.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
O que ajunta no verão é filho entendido, mas o que dorme na sega é filho que faz envergonhar.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Bençãos há sobre a cabeça do justo, mas a violência cobre a boca dos ímpios.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
A memória do justo é abençoada, mas o nome dos ímpios apodrecerá.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
O sábio de coração aceita os mandamentos, mas o louco de lábios será transtornado.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Quem anda em sinceridade, anda seguro; mas o que perverte os seus caminhos será conhecido.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
O que acena com os olhos dá dores, e o tolo de lábios será transtornado.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
A boca do justo é fonte de vida, mas a boca dos ímpios cobre a violência.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
O ódio excita contendas, mas o amor cobre todas as transgressões.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
Nos lábios do entendido se acha a sabedoria, mas a vara é para as costas do falto de entendimento.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Os sábios escondem a sabedoria; mas a boca do tolo está perto da ruína.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
A fazenda do rico é a cidade da sua fortaleza: a pobreza dos pobres é a sua ruína.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
A obra do justo conduz à vida, as novidades do ímpio ao pecado.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
O caminho para a vida é daquele que guarda a correção, mas o que deixa a repreensão faz errar.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
O que encobre o ódio tem lábios falsos, e o que produz má fama é um insensato.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Na multidão de palavras não há falta de transgressão, mas o que modera os seus lábios é prudente.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
Prata escolhida é a língua do justo: o coração dos ímpios é de nenhum preço.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Os lábios do justo apascentam a muitos, mas os tolos, por falta de entendimento, morrem.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
A benção do Senhor é a que enriquece; e não lhe acrescenta dores.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Como brincadeira é para o tolo fazer abominação, mas sabedoria para o homem entendido.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
O temor do ímpio virá sobre ele, mas o desejo dos justos Deus lhe cumprirá.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Como passa a tempestade, assim o ímpio mais não é; mas o justo tem perpétuo fundamento.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Como vinagre para os dentes, como o fumo para os olhos, assim é o preguiçoso para aqueles que o mandam.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
O temor do Senhor aumenta os dias, mas os anos dos ímpios serão abreviados.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
A esperança dos justos é alegria, mas a expectação dos ímpios perecerá.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
O caminho do Senhor é fortaleza para os retos, mas ruína será para os que obram iniquidade.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
O justo nunca jamais será abalado, mas os ímpios não habitarão a terra.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
A boca do justo em abundância produz sabedoria, mas a língua da perversidade será desarreigada.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Os beiços do justo sabem o que agrada, mas a boca dos ímpios anda cheia de perversidades.