< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Filius sapiens lætificat patrem: filius vero stultus mœstitia est matris suæ.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Nil proderunt thesauri impietatis: iustitia vero liberabit a morte.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Non affliget Dominus fame animam iusti, et insidias impiorum subvertet.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Egestatem operata est manus remissa: manus autem fortium divitias parat. Qui nititur mendaciis, hic pascit ventos: idem autem ipse sequitur aves volantes.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Qui congregat in messe, filius sapiens est: qui autem stertit æstate, filius confusionis.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Benedictio Domini super caput iusti: os autem impiorum operit iniquitas.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
Memoria iusti cum laudibus: et nomen impiorum putrescet.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Sapiens corde præcepta suscipit: stultus cæditur labiis.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Qui ambulat simpliciter, ambulat confidenter: qui autem depravat vias suas, manifestus erit.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Qui annuit oculo, dabit dolorem: et stultus labiis verberabitur.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Vena vitæ, os iusti: et os impiorum operit iniquitatem.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Odium suscitat rixas: et universa delicta operit charitas.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
In labiis sapientis invenitur sapientia: et virga in dorso eius qui indiget corde.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Sapientes abscondunt scientiam: os autem stulti confusioni proximum est.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
Substantia divitis, urbs fortitudinis eius: pavor pauperum, egestas eorum.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Opus iusti ad vitam: fructus autem impii ad peccatum.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Via vitæ, custodienti disciplinam: qui autem increpationes relinquit, errat.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Abscondunt odium labia mendacia: qui profert contumeliam, insipiens est.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
In multiloquio non deerit peccatum: qui autem moderatur labia sua prudentissimus est.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
Argentum electum, lingua iusti: cor autem impiorum pro nihilo.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Labia iusti erudiunt plurimos: qui autem indocti sunt, in cordis egestate morientur.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
Benedictio Domini divites facit, nec sociabitur eis afflictio.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Quasi per risum stultus operatur scelus: sapientia autem est viro prudentia.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Quod timet impius, veniet super eum: desiderium suum iustus dabitur.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Quasi tempestas transiens non erit impius: iustus autem quasi fundamentum sempiternum.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Sicut acetum dentibus, et fumus oculis, sic piger his, qui miserunt eum.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
Timor Domini apponet dies: et anni impiorum breviabuntur.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
Expectatio iustorum lætitia: spes autem impiorum peribit.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
Fortitudo simplicis via Domini: et pavor his, qui operantur malum.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Iustus in æternum non commovebitur: impii autem non habitabunt super terram.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
Os iusti parturiet sapientiam: lingua pravorum peribit.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Labia iusti considerant placita: et os impiorum perversa.

< Mithali 10 >