< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
ソロモンの箴言。知恵ある子は父を喜ばせ、愚かな子は母の悲しみとなる。
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
不義の宝は益なく、正義は人を救い出して、死を免れさせる。
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
主は正しい人を飢えさせず、悪しき者の欲望をくじかれる。
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
手を動かすことを怠る者は貧しくなり、勤め働く者の手は富を得る。
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
夏のうちに集める者は賢い子であり、刈入れの時に眠る者は恥をきたらせる子である。
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
正しい者のこうべには祝福があり、悪しき者の口は暴虐を隠す。
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
正しい者の名はほめられ、悪しき者の名は朽ちる。
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
心のさとき者は戒めを受ける、むだ口をたたく愚かな者は滅ぼされる。
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
まっすぐに歩む者の歩みは安全である、しかし、その道を曲げる者は災にあう。
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
目で、めくばせする者は憂いをおこし、あからさまに、戒める者は平和をきたらせる。
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
正しい者の口は命の泉である、悪しき者の口は暴虐を隠す。
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
憎しみは、争いを起し、愛はすべてのとがをおおう。
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
さとき者のくちびるには知恵があり、知恵のない者の背にはむちがある。
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
知恵ある者は知識をたくわえる、愚かな者のむだ口は、今にも滅びをきたらせる。
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
富める者の宝は、その堅き城であり、貧しい者の乏しきは、その滅びである。
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
正しい者の受ける賃銀は命に導き、悪しき者の利得は罪に至る。
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
教訓を守る者は命の道にあり、懲しめを捨てる者は道をふみ迷う。
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
憎しみを隠す者には偽りのくちびるがあり、そしりを口に出す者は愚かな者である。
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
言葉が多ければ、とがを免れない、自分のくちびるを制する者は知恵がある。
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
正しい者の舌は精銀である、悪しき者の心は価値が少ない。
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
正しい者のくちびるは多くの人を養い、愚かな者は知恵がなくて死ぬ。
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
主の祝福は人を富ませる、主はこれになんの悲しみをも加えない。
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
愚かな者は、戯れ事のように悪を行う、さとき人には賢い行いが楽しみである。
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
悪しき者の恐れることは自分に来り、正しい者の願うことは与えられる。
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
あらしが通りすぎる時、悪しき者は、もはや、いなくなり、正しい者は永久に堅く立てられる。
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
なまけ者は、これをつかわす者にとっては、酢が歯をいため、煙が目を悩ますようなものだ。
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
主を恐れることは人の命の日を多くする、悪しき者の年は縮められる。
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
正しい者の望みは喜びに終り、悪しき者の望みは絶える。
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
主は、まっすぐに歩む者には城であり、悪を行う者には滅びである。
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
正しい者はいつまでも動かされることはない、悪しき者は、地に住むことができない。
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
正しい者の口は知恵をいだし、偽りの舌は抜かれる。
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
正しい者のくちびるは喜ばるべきことをわきまえ、悪しき者の口は偽りを語る。

< Mithali 10 >