< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Proverbes de Salomon. L'enfant sage réjouit son père; mais l'enfant insensé est le chagrin de sa mère.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Les trésors de méchanceté ne profitent point; mais la justice délivre de la mort.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
L'Éternel ne permet pas que le juste souffre de la faim; mais il repousse l'avidité des méchants.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
La main paresseuse appauvrit; mais la main des diligents enrichit.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Celui qui amasse en été est un fils prudent; celui qui dort pendant la moisson est un fils qui fait honte.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Il y a des bénédictions sur la tête du juste; mais la violence fermera la bouche aux méchants.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
La mémoire du juste sera en bénédiction; mais le nom des méchants tombera en pourriture.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Celui qui a le cœur sage, reçoit les avertissements; mais celui qui a les lèvres insensées, tombera.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Celui qui marche dans l'intégrité, marche en assurance; mais celui qui pervertit ses voies, sera découvert.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Celui qui cligne de l'œil cause du trouble; et celui qui a les lèvres insensées, court à sa perte.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
La bouche du juste est une source de vie; mais la violence fermera la bouche aux méchants.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
La haine excite les querelles; mais la charité couvre toutes les fautes.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
La sagesse se trouve sur les lèvres de l'homme sage; mais la verge est pour le dos de celui qui est dépourvu de sens.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Les sages tiennent la science en réserve; mais la bouche de l'insensé est une ruine prochaine.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
Les biens du riche sont sa ville forte; mais la pauvreté des misérables est leur ruine.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
L'œuvre du juste conduit à la vie; mais le fruit du méchant est le péché.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Celui qui garde l'instruction, est dans le chemin de la vie; mais celui qui oublie la correction, s'égare.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Celui qui dissimule la haine a des lèvres trompeuses; et celui qui répand la calomnie, est un insensé.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Où il y a beaucoup de paroles, il ne manque pas d'y avoir du péché; mais celui qui retient ses lèvres est prudent.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
La langue du juste est un argent de choix; mais le cœur des méchants vaut peu de chose.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Les lèvres du juste nourrissent beaucoup d'hommes; mais les insensés mourront, faute de sens.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
C'est la bénédiction de l'Éternel qui enrichit, et il n'y joint aucune peine.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Faire le mal est la joie de l'insensé; la sagesse est celle de l'homme prudent.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Ce que le méchant craint, lui arrivera; mais Dieu accordera aux justes ce qu'ils désirent.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Comme le tourbillon passe, ainsi le méchant disparaît; mais le juste s'appuie sur un fondement éternel.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Ce que le vinaigre est aux dents, et la fumée aux yeux, tel est le paresseux à ceux qui l'envoient.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
La crainte de l'Éternel multiplie les jours; mais les années des méchants seront retranchées.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
L'espérance des justes est la joie; mais l'attente des méchants périra.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
La voie de l'Éternel est la force de l'homme intègre; mais elle est la ruine des ouvriers d'iniquité.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Le juste ne sera jamais ébranlé; mais les méchants n'habiteront point sur la terre.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
La bouche du juste produira la sagesse; mais la langue perverse sera retranchée.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Les lèvres du juste connaissent ce qui est agréable; mais la bouche des méchants n'est que perversité.

< Mithali 10 >