< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Le fils sage réjouit son père; le fils insensé est le chagrin de sa mère.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Les trésors ne serviront de rien aux pervers; mais l'équité délivrera de la mort.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Le Seigneur ne laissera pas mourir de faim l'âme du juste; mais Il détruira la vie des impies.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
L'indigence abaisse l'homme; mais des mains fortes enrichissent. Le fils bien enseigné sera sage, et il se fera servir par l'insensé.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Le fils prudent n'a point à souffrir de la grande chaleur; mais le fils pervers est un épi consumé par le vent pendant la moisson.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
La bénédiction du Seigneur est sur la tête du juste; mais des deuils imprévus couvrent la tête des impies.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
La mémoire des justes a la louange pour elle; mais le nom des impies s'éteint.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Le sage recueille les commandements en son cœur; mais l'homme aux lèvres indiscrètes prend des détours et trébuche.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Celui qui marche en sa simplicité, marche avec confiance; celui qui se détourne dans ses voies sera découvert.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Celui qui approuve d'un regard rusé prépare toute sorte de chagrins aux hommes; mais celui qui réprimande avec franchise est un pacificateur.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Il y a une source de vie dans la main du juste; mais la perdition est cachée dans la bouche des impies.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
La haine suscite la discorde; l'amitié protège tous ceux qui n'aiment point les querelles.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
Celui dont les lèvres professent la sagesse frappe d'une verge l'homme privé de sens.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Les sages cachent leur science; mais la bouche du téméraire le conduit à la confusion.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
La fortune des riches est leur forteresse, et la pauvreté est pour les impies le brisement du cœur.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Les œuvres des justes donnent la vie; mais les fruits des impies sont autant de péchés.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
L'instruction garde droites les voies de la vie; mais l'instruction superficielle égare.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Les paroles bien mesurées recèlent la haine; mais ceux qui se répandent en injures sont des plus insensés.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Par la multitude des paroles, tu n'éviteras pas le péché; par la discrétion des lèvres, tu seras sage.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
La langue du juste est de l'argent pur; mais le cœur de l'impie est sans valeur.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Les lèvres des justes savent des vérités sublimes; les insensés meurent dans l'indigence.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
La bénédiction du Seigneur est sur la tête du juste; elle l'enrichit, et il ne s'y joindra aucune tristesse de cœur.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
L'insensé fait le mal en riant; la sagesse de l'homme enfante la prudence.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
L'impie est emporté dans sa perdition; mais le désir du juste est exaucé.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Comme la tempête passe, ainsi l'impie disparaît; le juste s'en détourne, et il est sauvé pour tous les siècles.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Comme le fruit vert nuit aux dents et la fumée aux yeux, de même l'iniquité nuit aux injustes.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
La crainte du Seigneur multiplie les jours; mais les années des impies sont abrégées.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
La joie du juste est durable; l'espérance des impies périra.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
La crainte du Seigneur est la forteresse du saint; mais l'affection vient à ceux qui font le mal.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Le juste ne se relâchera jamais; mais les impies n'habiteront pas la terre.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
La bouche du juste distille la sagesse; la langue des impies périra.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Les lèvres du juste distillent la grâce; la bouche des impies, la perversité.

< Mithali 10 >