< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Paraboles de Salomon. Le fils sage fait la joie de son père, et le fils insensé le chagrin de sa mère.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Les trésors acquis par le crime ne profitent pas, mais la justice délivre de la mort.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Yahweh ne laisse pas le juste souffrir de la faim, mais il repousse la convoitise du méchant.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Il s'appauvrit celui qui travaille d'une main paresseuse, mais la main des diligents amasse des richesses.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Celui qui recueille pendant l'été est un fils prudent; celui qui dort au temps de la moisson est un fils de confusion.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
La bénédiction vient sur la tête du juste, mais l'injustice couvre la bouche des méchants.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
La mémoire du juste est en bénédiction, mais le nom des méchants tombe en pourriture.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Celui qui est sage de cœur reçoit les préceptes, mais celui qui est insensé des lèvres va à sa perte.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Celui qui marche dans l'intégrité marche en confiance, mais celui qui prend des voies tortueuses sera découvert.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Celui qui cligne les yeux sera une cause de chagrin, et celui qui est insensé des lèvres va à sa perte.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
La bouche du juste est une source de vie, mais l'injustice couvre la bouche du méchant.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
La haine suscite des querelles, mais l'amour couvre toutes les fautes.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
Sur les lèvres de l'homme intelligent se trouve la sagesse, mais la verge est pour le dos de celui qui manque de sens.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Les sages tiennent la sagesse en réserve, mais la bouche de l'insensé est un malheur prochain.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
La fortune est pour le riche sa place forte, le malheur des misérables, c'est leur pauvreté.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
L'œuvre du juste est pour la vie, le gain du méchant est pour le péché.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Celui qui prend garde à l'instruction prend le chemin de la vie; mais celui qui oublie la réprimande s'égare.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Celui qui cache la haine a des lèvres menteuses, et celui qui répand la calomnie est un insensé.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
L'abondance de paroles ne va pas sans péché, mais celui qui retient ses lèvres est un homme prudent.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
La langue du juste est un argent de choix; le cœur des méchants est de peu de prix.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Les lèvres du juste nourrissent beaucoup d'hommes, mais les insensés meurent par défaut d'intelligence.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
C'est la bénédiction du Seigneur qui procure la richesse, et la peine que l'on prend n'y ajoute rien.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Commettre le crime paraît un jeu à l'insensé; il en est de même de la sagesse pour l'homme intelligent.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Ce que redoute le méchant lui arrive, et Dieu accorde au juste ce qu'il désire.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Comme passe le tourbillon, le méchant disparaît; le juste est établi sur un fondement éternel.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Ce que le vinaigre est aux dents et la fumée aux yeux, tel est le paresseux pour ceux qui l'envoient.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
La crainte de Yahweh augmente les jours, mais les années des méchants sont abrégées.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
L'attente des justes n'est que joie, mais l'espérance des méchants périra.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
La voie de Yahweh est un rempart pour le juste, mais elle est une ruine pour ceux qui font le mal.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Le juste ne chancellera jamais, mais les méchants n'habiteront pas la terre.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
La bouche du juste produit la sagesse, et la langue perverse sera arrachée.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Les lèvres du juste connaissent la grâce, et la bouche des méchants la perversité.

< Mithali 10 >