< Mithali 10 >
1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Les proverbes de Salomon. Un fils sage fait un père heureux; mais un fils insensé apporte du chagrin à sa mère.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Les trésors de la méchanceté ne servent à rien, mais la justice délivre de la mort.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Yahvé ne permettra pas que l'âme du juste ait faim, mais il repousse le désir des méchants.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Celui qui travaille d'une main paresseuse devient pauvre, mais la main du diligent apporte la richesse.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Celui qui recueille en été est un fils sage, mais celui qui dort pendant la moisson est un fils qui fait honte.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Les bénédictions sont sur la tête des justes, mais la violence couvre la bouche des méchants.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
La mémoire des justes est bénie, mais le nom des méchants pourrira.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Les sages de cœur acceptent les commandements, mais un imbécile bavard tombera.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Celui qui marche sans reproche marche sûrement, mais celui qui pervertit ses voies sera découvert.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Celui qui fait un clin d'œil provoque la tristesse, mais un imbécile bavard tombera.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
La bouche du juste est une source de vie, mais la violence couvre la bouche des méchants.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
La haine suscite des querelles, mais l'amour couvre tous les maux.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
La sagesse se trouve sur les lèvres de celui qui a du discernement, mais la verge est pour le dos de celui qui est dépourvu d'intelligence.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Les sages accumulent des connaissances, mais la bouche de l'insensé est proche de la ruine.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
La richesse du riche, c'est sa ville forte. La destruction des pauvres est leur pauvreté.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Le travail des justes mène à la vie. L'augmentation des méchants conduit au péché.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Il est dans la voie de la vie celui qui tient compte de la correction, mais celui qui délaisse la réprimande égare les autres.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Celui qui cache la haine a des lèvres mensongères. Celui qui profère une calomnie est un fou.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Dans la multitude des paroles, la désobéissance ne manque pas, mais celui qui retient ses lèvres fait preuve de sagesse.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
La langue des justes est comme de l'argent précieux. Le cœur des méchants est de peu de valeur.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Les lèvres des justes en nourrissent beaucoup, mais les insensés meurent par manque de compréhension.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
La bénédiction de Yahvé apporte la richesse, et il n'y ajoute aucun problème.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
C'est un plaisir pour l'insensé de faire le mal, mais la sagesse est un homme de plaisir de l'intelligence.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Ce que les méchants craignent les rattrapera, mais le désir des justes sera exaucé.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Quand le tourbillon passe, le méchant n'est plus; mais les justes restent fermes pour toujours.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Comme du vinaigre pour les dents, et comme de la fumée pour les yeux, Il en est de même du paresseux pour ceux qui l'envoient.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
La crainte de Yahvé prolonge les jours, mais les années des méchants seront abrégées.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
La perspective des justes est la joie, mais l'espoir des méchants périra.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
La voie de Yahvé est une forteresse pour les hommes droits, mais c'est une destruction pour les ouvriers de l'iniquité.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Les justes ne seront jamais supprimés, mais les méchants n'habiteront pas le pays.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
La bouche du juste produit la sagesse, mais la langue perverse sera coupée.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Les lèvres des justes savent ce qui est acceptable, mais la bouche des méchants est perverse.