< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Salomon sananlaskut. Viisas poika on isällensä iloksi, mutta tyhmä poika on äidillensä murheeksi.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Vääryyden aarteet eivät auta, mutta vanhurskaus vapahtaa kuolemasta.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Herra ei salli vanhurskaan nälkää nähdä, mutta jumalattomien himon hän luotansa työntää.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Köyhtyy, joka laiskasti kättä käyttää, mutta ahkerain käsi rikastuttaa.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Taitava poika kokoaa kesällä, kunnoton poika elonaikana nukkuu.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Siunaus on vanhurskaan pään päällä, mutta väkivaltaa kätkee jumalattomien suu.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
Vanhurskaan muistoa siunataan, mutta jumalattomien nimi lahoaa.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Viisassydäminen ottaa käskyt varteen, mutta hulluhuulinen kukistuu.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Joka nuhteettomasti vaeltaa, vaeltaa turvassa, jonka tiet ovat väärät, se joutuu ilmi.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Joka silmää iskee, saa aikaan tuskaa, ja hulluhuulinen kukistuu.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Vanhurskaan suu on elämän lähde, mutta jumalattomien suu kätkee väkivaltaa.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Viha virittää riitoja, mutta rakkaus peittää rikkomukset kaikki.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
Ymmärtäväisen huulilta löytyy viisaus, mutta joka on mieltä vailla, sille vitsa selkään!
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Viisaat kätkevät, minkä tietävät, mutta hullun suu on läheinen turmio.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
Rikkaan tavara on hänen vahva kaupunkinsa, mutta vaivaisten köyhyys on heidän turmionsa.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Vanhurskaan hankkima on elämäksi, jumalattoman saalis koituu synniksi.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Kuritusta noudattava on elämän tiellä, mutta nuhteet hylkäävä eksyy.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Joka salavihaa pitää, sen huulilla on valhe, ja joka parjausta levittää, on tyhmä.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Missä on paljon sanoja, siinä ei syntiä puutu; mutta joka huulensa hillitsee, se on taitava.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
Vanhurskaan kieli on valituin hopea, jumalattomien äly on tyhjän veroinen.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Vanhurskaan huulet kaitsevat monia, mutta hullut kuolevat mielettömyyteensä.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
Herran siunaus rikkaaksi tekee, ei oma vaiva siihen mitään lisää.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Tyhmälle on iloksi ilkityön teko, mutta ymmärtäväiselle miehelle viisaus.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Mitä jumalaton pelkää, se häntä kohtaa; mutta mitä vanhurskaat halajavat, se annetaan.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Tuulispään käytyä ei jumalatonta enää ole, mutta vanhurskaan perustus pysyy iäti.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Mitä hapan hampaille ja savu silmille, sitä laiska lähettäjillensä.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
Herran pelko elinpäiviä jatkaa, mutta jumalattomien vuodet lyhenevät.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
Vanhurskasten odotus koituu iloksi, mutta jumalattomien toivo hukkuu.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
Herran johdatus on nuhteettoman turva, mutta väärintekijäin turmio.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Vanhurskas ei ikinä horju, mutta jumalattomat eivät saa asua maassa.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
Vanhurskaan suu kasvaa viisauden hedelmän, mutta kavala kieli hävitetään.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Vanhurskaan huulet tietävät, mikä otollista on, mutta jumalattomien suu on sulaa kavaluutta.

< Mithali 10 >