< Mithali 10 >
1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Proverbs of Solomon. A wise son causeth a father to rejoice, And a foolish son [is] an affliction to his mother.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Treasures of wickedness profit not, And righteousness delivereth from death.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Jehovah causeth not the soul of the righteous to hunger, And the desire of the wicked He thrusteth away.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Poor [is] he who is working — a slothful hand, And the hand of the diligent maketh rich.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Whoso is gathering in summer [is] a wise son, Whoso is sleeping in harvest [is] a son causing shame.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Blessings [are] for the head of the righteous, And the mouth of the wicked cover doth violence.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
The remembrance of the righteous [is] for a blessing, And the name of the wicked doth rot.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
The wise in heart accepteth commands, And a talkative fool kicketh.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Whoso is walking in integrity walketh confidently, And whoso is perverting his ways is known.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Whoso is winking the eye giveth grief, And a talkative fool kicketh.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
A fountain of life [is] the mouth of the righteous, And the mouth of the wicked cover doth violence.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Hatred awaketh contentions, And over all transgressions love covereth.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
In the lips of the intelligent is wisdom found, And a rod [is] for the back of him who is lacking understanding.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
The wise lay up knowledge, and the mouth of a fool [is] near ruin.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
The wealth of the rich [is] his strong city, The ruin of the poor [is] their poverty.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
The wage of the righteous [is] for life, The increase of the wicked for sin.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
A traveller to life [is] he who is keeping instruction, And whoso is forsaking rebuke is erring.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Whoso is covering hatred with lying lips, And whoso is bringing out an evil report is a fool.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
In the abundance of words transgression ceaseth not, And whoso is restraining his lips [is] wise.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
The tongue of the righteous [is] chosen silver, The heart of the wicked — as a little thing.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
The lips of the righteous delight many, And fools for lack of heart die.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
The blessing of Jehovah — it maketh rich, And He addeth no grief with it.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
To execute inventions [is] as play to a fool, And wisdom to a man of understanding.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
The feared thing of the wicked it meeteth him, And the desire of the righteous is given.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
As the passing by of a hurricane, So the wicked is not, And the righteous is a foundation age-during.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
As vinegar to the teeth, And as smoke to the eyes, So [is] the slothful to those sending him.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
The fear of Jehovah addeth days, And the years of the wicked are shortened.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
The hope of the righteous [is] joyful, And the expectation of the wicked perisheth.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
The way of Jehovah [is] strength to the perfect, And ruin to workers of iniquity.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
The righteous to the age is not moved, And the wicked inhabit not the earth.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
The mouth of the righteous uttereth wisdom, And the tongue of frowardness is cut out.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
The lips of the righteous know a pleasing thing, And the mouth of the wicked perverseness!