< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
The proverbs of Solomon. A wise son maketh a glad father: but a foolish son [is] the heaviness of his mother.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Treasures of wickedness profit nothing: but righteousness delivereth from death.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
The LORD will not suffer the soul of the righteous to famish: but he casteth away the substance of the wicked.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
He becometh poor that dealeth [with] a slack hand: but the hand of the diligent maketh rich.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
He that gathereth in summer [is] a wise son: [but] he that sleepeth in harvest [is] a son that causeth shame.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Blessings [are] upon the head of the just: but violence covereth the mouth of the wicked.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
The memory of the just [is] blessed: but the name of the wicked shall perish.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
The wise in heart will receive commandments: but a prating fool shall fall.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
He that walketh uprightly walketh surely: but he that perverteth his ways shall be known.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
He that winketh with the eye causeth sorrow: but a prating fool shall fall.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
The mouth of a righteous [man is] a well of life: but violence covereth the mouth of the wicked.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Hatred stirreth up strifes: but love covereth all sins.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
In the lips of him that hath understanding wisdom is found: but a rod [is] for the back of him that is void of understanding.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Wise [men] lay up knowledge: but the mouth of the foolish [is] near destruction.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
The rich man's wealth [is] his strong city: the destruction of the poor [is] their poverty.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
The labor of the righteous [tendeth] to life: the fruit of the wicked to sin.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
He [is in] the way of life that keepeth instruction: but he that refuseth reproof erreth.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
He that hideth hatred [with] lying lips, and he that uttereth a slander, [is] a fool.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
In the multitude of words there wanteth not sin: but he that restraineth his lips [is] wise.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
The tongue of the just [is as] choice silver: the heart of the wicked [is] little worth.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
The lips of the righteous feed many: but fools die for want of wisdom.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
The blessing of the LORD, it maketh rich, and he addeth no sorrow with it.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
[It is] as sport to a fool to do mischief: but a man of understanding hath wisdom.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
The fear of the wicked, it shall come upon him: but the desire of the righteous shall be granted.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
As the whirlwind passeth, so [is] the wicked no [more]: but the righteous [is] an everlasting foundation.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
As vinegar to the teeth, and as smoke to the eyes, so [is] the sluggard to them that send him.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
The fear of the LORD prolongeth days: but the years of the wicked shall be shortened.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
The hope of the righteous [shall be] gladness: but the expectation of the wicked shall perish.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
The way of the LORD [is] strength to the upright: but destruction [shall be] to the workers of iniquity.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
The righteous shall never be removed: but the wicked shall not inhabit the earth.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
The mouth of the just bringeth forth wisdom: but the froward tongue shall be cut out.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
The lips of the righteous know what is acceptable: but the mouth of the wicked [speaketh] frowardness.

< Mithali 10 >