< Mithali 10 >
1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
The proverbs of Solomon. A wise son causeth [his] father to rejoice; but a foolish son is the grief of his mother.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Treasures of wickedness will not profit aught; but righteousness will deliver from death.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
The Lord will not suffer the soul of the righteous to famish; but the sinful desires of the wicked will he cast away.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
He becometh poor that laboreth with an indolent hand, but the hand of the diligent maketh rich.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
He that gathereth in summer is an intelligent son; [but] he that sleepeth in harvest is a son that causeth shame.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Blessings come upon the head of the righteous; but the mouth of the wicked covereth violence.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
The memory of the just is [destined] to be blessed; but the name of the wicked shall rot.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
The wise in heart will accept commandments; but he that is a fool in his speaking will stumble.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
He that walketh uprightly ever walketh securely; but he that perverteth his ways will be punished.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
He that winketh with the eye causeth vexation; and he that is a fool in his speaking will stumble.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
A source of life is the mouth of the righteous; but the mouth of the wicked covereth violence.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Hatred stirreth up strifes; but love throweth a cover over all transgressions.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
On the lips of the man of understanding there is found wisdom: but a rod is for the back of him that is void of sense.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Wise men treasure up knowledge; but the mouth of the foolish is an approaching terror.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
The wealth of the rich man is his strong town: the terror of the poor is their poverty.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
The labor of the righteous [tendeth] to life: the product of the wicked is for sin.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
On the way unto life is he that observeth correction; but he that forsaketh reproof is in error.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
He that hideth hatred hath lips of falsehood; and he that spreadeth abroad an evil report, is a fool.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
In a multitude of words transgression cannot be avoided; but he that refraineth his lips is intelligent.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
[Like] choice silver is the tongue of the righteous: the heart of the wicked is worth but very little.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
The lips of the righteous feed many: but fools die through lack of sense.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
The blessing of the Lord it is which maketh rich, and painful labor addeth nothing thereto.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
It is as sport to a fool to do wicked deeds; but a man of understanding hath wisdom.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
What the wicked dreadeth, that will come upon him: but the longing of the righteous will God grant.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
As the whirlwind passeth by, the wicked is no more; but the righteous is an everlasting foundation.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
As vinegar is to the teeth, and as smoke is to the eyes: so is the sluggard to those that send him.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
The fear of the Lord increaseth [man's] days; but the years of the wicked will be shortened.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
The expectation of the righteous is joy; but the hope of the wicked shall perish.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
The way of the Lord is a stronghold to the upright; but terror is destined to the workers of injustice.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
The righteous shall never be removed; but the wicked shall not inhabit the earth.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
The mouth of the just uttereth wisdom; but the tongue of perverseness shall be cut out.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
The lips of the righteous know [how to obtain] favor; but the mouth of the wicked [speaketh] perverseness.