< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
A wise son makes [his] father glad: but a foolish son is a grief to his mother.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Treasures shall not profit the lawless: but righteousness shall deliver from death.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
The Lord will not famish a righteous soul: but he will overthrow the life of the ungodly.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Poverty brings a man low: but the hands of the vigorous make rich. A son who is instructed shall be wise, and shall use the fool for a servant.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
A wise son is saved from heat: but a lawless son is blighted of the winds in harvest.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
The blessing of the Lord is upon the head of the just: but untimely grief shall cover the mouth of the ungodly.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
The memory of the just is praised; but the name of the ungodly [man] is extinguished.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
A wise man in heart will receive commandments; but he that is unguarded in his lips shall be overthrown in his perverseness.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
He that walks simply, walks confidently; but he that perverts his ways shall be known.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
He that winks with his eyes deceitfully, procures griefs for men; but he that reproves boldly is a peacemaker.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
[There is] a fountain of life in the hand of a righteous man; but destruction shall cover the mouth of the ungodly.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Hatred stirs up strife; but affection covers all that do not love strife.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
He that brings forth wisdom from his lips smites the fool with a rod.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
The wise will hide discretion; but the mouth of the hasty draws near to ruin.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
The wealth of rich men is a strong city; but poverty is the ruin of the ungodly.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
The works of the righteous produce life; but the fruits of the ungodly [produce] sins.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Instruction keeps the right ways of life; but instruction unchastened goes astray.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Righteous lips cover enmity; but they that utter railings are most foolish.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
By a multitude of words you shall not escape sin; but if you refrain your lips you will be prudent.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
The tongue of the just is tried silver; but the heart of the ungodly shall fail.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
The lips of the righteous know sublime [truths]: but the foolish die in lack.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
The blessing of the Lord is upon the head of the righteous; it enriches [him], and grief of heart shall not be added to [it].
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
A fool does mischief in sport; but wisdom brings forth prudence for a man.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
The ungodly is engulfed in destruction; but the desire of the righteous is acceptable.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
When the storm passes by, the ungodly vanishes away; but the righteous turns aside and escapes for ever.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
As a sour grape is hurtful to the teeth, and smoke to the eyes, so iniquity hurts those that practise it.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
The fear of the Lord adds [length] of days: but the years of the ungodly shall be shortened.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
Joy rests long with the righteous: but the hope of the ungodly shall perish.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
The fear of the Lord is a strong hold of the saints: but ruin [comes] to them that work wickedness.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
The righteous shall never fail: but the ungodly shall not dwell in the earth.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
The mouth of the righteous drops wisdom: but the tongue of the unjust shall perish.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
The lips of just men drop grace: but the mouth of the ungodly is perverse.

< Mithali 10 >