< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
A wise son maketh the father glad: but a foolish son is the sorrow of his mother.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Treasures of wickedness shall profit nothing: but justice shall deliver from death.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
The Lord will not afflict the soul of the just with famine, and he will disappoint the deceitful practices of the wicked.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
The slothful hand hath wrought poverty: but the hand of the industrious getteth riches. He that trusteth to lies feedeth the winds: and the same runneth after birds that fly away.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
He that gathered in the harvest is a wise son: but he that snorteth in the summer, is the son of confusion.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
The blessing of the Lord is upon the head of the just: but iniquity covereth the mouth of the wicked.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
The memory of the just is with praises: and the name of the wicked shall rot.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
The wise of heart receiveth precepts: a fool is beaten with lips.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
He that walketh sincerely, walketh confidently: but he that perverteth his ways, shall be manifest.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
He that winketh with the eye shall cause sorrow: and the foolish in lips shall be beaten.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
The mouth of the just is a vein of life: and the mouth of the wicked covereth iniquity.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Hatred stirreth up strifes: and charity covereth all sins.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
In the lips of the wise is wisdom found: and a rod on the back of him that wanteth sense.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Wise men lay up knowledge: but the mouth of the fool is next to confusion.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
The substance of a rich man is the city of his strength: the fear of the poor is their poverty.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
The work of the just is unto life: but the fruit of the wicked, unto sin.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
The way of life, to him that observeth correction: but he that forsaketh reproofs goeth astray.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Lying lips hide hatred: he that uttereth reproach is foolish.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
In the multitude of words there shall not want sin: but he that refraineth his lips is most wise.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
The tongue of the just is as choice silver: but the heart of the wicked is nothing worth.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
The lips of the just teach many: but they that are ignorant, shall die in the want of understanding.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
The blessing of the Lord maketh men rich: neither shall affliction be joined to them.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
A fool worketh mischief as it were for sport: but wisdom is prudence to a man.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
That which the wicked feareth, shall come upon him: to the just their desire shall be given.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
As a tempest that passeth, so the wicked shall be no more: but the just is as an everlasting foundation.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
As vinegar to the teeth, and smoke to the eyes, so is the sluggard to them that sent him.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
The fear of the Lord shall prolong days: and the years of the wicked shall be shortened.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
The expectation of the just is joy; but the hope of the wicked shall perish.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
The strength of the upright is the way of the Lord: and fear to them that work evil.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
The just shall never be moved: but the wicked shall not dwell on the earth.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
The mouth of the just shall bring forth wisdom: the tongue of the perverse shall perish.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
The lips of the just consider what is acceptable: and the mouth of the wicked uttereth perverse things.

< Mithali 10 >