< Mithali 10 >
1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
En viis Søn glæder sin Fader, men en daarlig Søn er sin Moders Bedrøvelse.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Ugudeliges Liggendefæ gavner intet, men Retfærdighed redder fra Døden.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Herren lader ikke den retfærdiges Sjæl hungre, men de ugudeliges Begærlighed støder han tilbage.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Den, som arbejder med lad Haand, bliver fattig; men de flittiges Haand gør rig.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Den, som samler om Sommeren, er en klog Søn; den, som sover om Høsten, er en Søn, der gør Skam.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Velsignelser ere over den retfærdiges Hoved, men Vold skjuler de ugudeliges Mund.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
Den retfærdiges Ihukommelse er til Velsignelse; men de ugudeliges Navn smuldrer hen.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Den, som er viis af Hjerte, tager imod Budene; men den, som er en Daare i sin Mund, styrtes.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Den, som vandrer i Oprigtighed, vandrer tryggelig; men den, som gaar Krogveje, bliver røbet.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Den, som giver Vink med Øjet, foraarsager Krænkelse; og den, som er en Daare i sin Mund, styrtes.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Den retfærdiges Mund er Livets Kilde, men Vold skjuler de ugudeliges Mund.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Had opvækker Trætter, men Kærlighed skjuler alle Overtrædelser.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
Paa den forstandiges Læber findes Visdom; men en Kæp er for den uforstandiges Ryg.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
De vise gemme paa Kundskab; men for Daarens Mund er Undergang nær.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
Den riges Gods er hans faste Stad; men de fattiges Armod er deres egen Undergang.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Den retfærdiges Løn er til Livet; den ugudeliges Indtægt er til Synd.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
At bevare Tugt er Vej til Livet; men den, som lader Tilrettevisning fare, vildleder.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Den, som dølger Had, har falske Læber, og den, som bringer ondt Rygte ud, er en Daare.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Hvor mange Ord ere, der lader Overtrædelse ikke af; men den, som sparer sine Læber, er klog.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
Den retfærdiges Tunge er udsøgt Sølv; de ugudeliges Hjerte er intet værd.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Den retfærdiges Læber nære mange; men ved den uforstandige dø Daarer.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
Herrens Velsignelse gør rig, og han føjer ikke Smerte til den.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Det er for Daaren som en Leg, naar han gør en skændig Ting; men den forstandige Mand har Visdom.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Hvad den ugudelige frygter for, det skal komme over ham; men de retfærdiges Begæring skal Gud give ham.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Naar Hvirvelvinden farer forbi, saa er den ugudelige ikke mere; men en retfærdig har en evig Grundvold.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Som Eddike er for Tænderne, og som Røg er for Øjnene, saa er den lade for dem, som udsende ham.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
Herrens Frygt lægger Dage til; men de ugudeliges Aar forkortes.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
De retfærdiges Forventelse er Glæde, men de ugudeliges Haab forgaar.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
En fast Borg er Herrens Vej for den retskafne, men Fordærvelse for dem, som gøre Uret.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Den retfærdige skal ikke rokkes evindelig; men de ugudelige skulle ikke bo i Landet.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
Den retfærdiges Mund fremfører Visdom, men den Tunge, som taler forvendte Ting, skal udryddes.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Den retfærdiges Læber kende, hvad der er velbehageligt, men de ugudeliges Mund fremfører forvendte Ting.