< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Syn moudrý obveseluje otce, ale syn bláznivý zámutkem jest matce své.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Neprospívají pokladové bezbožně nabytí, ale spravedlnost vytrhuje od smrti.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Nedopustí lačněti Hospodin duši spravedlivého, statek pak bezbožných rozptýlí.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
K nouzi přivodí ruka lstivá, ruka pak pracovitých zbohacuje.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Kdo shromažďuje v létě, jest syn rozumný; kdož vyspává ve žni, jest syn, kterýž hanbu činí.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Požehnání jest nad hlavou spravedlivého, ale ústa bezbožných přikrývají ukrutnost.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
Památka spravedlivého požehnaná, ale jméno bezbožných smrdí.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Moudré srdce přijímá přikázaní, ale blázen od rtů svých padne.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Kdo chodí upřímě, chodí doufanlivě; kdož pak převrací cesty své, vyjeven bude.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Kdo mhourá okem, uvodí nesnáz; a kdož jest bláznivých rtů, padne.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Pramen života jsou ústa spravedlivého, ale ústa bezbožných přikrývají ukrutnost.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Nenávist vzbuzuje sváry, ale láska přikrývá všecka přestoupení.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
Ve rtech rozumného nalézá se moudrost, ale kyj na hřbetě blázna.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Moudří skrývají umění, úst pak blázna blízké jest setření.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
Zboží bohatého jest město pevné jeho, ale nouze jest chudých setření.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Práce spravedlivého jest k životu, nábytek pak bezbožných jest k hříchu.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Stezkou života jde, kdož přijímá trestání; ale kdož pohrdá domlouváním, bloudí.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Kdož přikrývá nenávist rty lživými, i kdož uvodí v lehkost, ten blázen jest.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Mnohé mluvení nebývá bez hříchu, kdož pak zdržuje rty své, opatrný jest.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
Stříbro výborné jest jazyk spravedlivého, ale srdce bezbožných za nic nestojí.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Rtové spravedlivého pasou mnohé, blázni pak pro bláznovství umírají.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
Požehnání Hospodinovo zbohacuje, a to beze všeho trápení.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Za žert jest bláznu činiti nešlechetnost, ale muž rozumný moudrosti se drží.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Čeho se bojí bezbožný, to přichází na něj; ale čehož žádají spravedliví, dává Bůh.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Jakož pomíjí vichřice, tak nestane bezbožníka, spravedlivý pak jest základ stálý.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Jako ocet zubům, a jako dým očima, tak jest lenivý těm, kteříž jej posílají.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
Bázeň Hospodinova přidává dnů, léta pak bezbožných ukrácena bývají.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
Očekávání spravedlivých jest potěšení, naděje pak bezbožných zahyne.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
Silou jest upřímému cesta Hospodinova, a strachem těm, kteříž činí nepravost.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Spravedlivý na věky se nepohne, bezbožní pak nebudou bydliti v zemi.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
Ústa spravedlivého vynášejí moudrost, ale jazyk převrácený vyťat bude.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Rtové spravedlivého znají, což jest Bohu libého, ústa pak bezbožných převrácené věci.

< Mithali 10 >