< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Mudar sin veseli oca, a lud je sin žalost majci svojoj.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Ne koristi krivo stečeno blago, dok pravednost izbavlja od smrti.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Ne dopušta Jahve da gladuje duša pravednika, ali odbija pohlepu opakih.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Lijena ruka osiromašuje čovjeka, a marljiva ga obogaćuje.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Tko sabira ljeti, razuman je sin, a tko hrče o žetvi, navlači sramotu.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Blagoslovi su nad glavom pravedniku, a usta opakih kriju nasilje.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
Pravednikov je spomen blagoslovljen, a opakom se ime proklinje.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
Tko je mudra srca, prima zapovijedi, dok brbljava luda propada.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Tko nedužno živi, hodi bez straha, a tko ide krivim putovima, poznat će se.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Tko žmirka okom, zadaje tugu, a tko ludo zbori, propada.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Pravednikova su usta izvor života, a opakomu usta kriju nasilje.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Mržnja izaziva svađu, a ljubav pokriva sve pogreške.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
Na usnama razumnoga nalazi se mudrost, a batina je za leđa nerazumna čovjeka.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Mudri kriju znanje, a luđakova su usta blizu propasti.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
Blago je bogatomu tvrdi grad, a ubogima je propast njihovo siromaštvo.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Pravednik prirađuje za život, a opaki prirađuje za grijeh.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Tko se naputka drži, na putu je života, a zabluđuje tko se na ukor ne osvrće.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Lažljive usne kriju mržnju, a tko klevetu širi, bezuman je!
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Obilje riječi ne biva bez grijeha, a tko zauzdava svoj jezik, razuman je.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
Pravednikov je jezik odabrano srebro, a razum opakoga malo vrijedi.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Pravednikove su usne hrana mnogima, a luđaci umiru s ludosti svoje.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
Gospodnji blagoslov obogaćuje i ne prati ga nikakva muka.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Bezumniku je radost učiniti sramotno djelo, a razumnu čovjeku biti mudar.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Čega se opaki boji, ono će ga stići, a pravednička se želja ispunjava.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Kad oluja prohuja, opakoga nestane, a pravednik ima temelj vječni.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Kakav je ocat zubima i dim očima, takav je ljenivac onima koji ga šalju.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
Strah Gospodnji umnaža dane, a opakima se prekraćuju godine.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
Pravedničko je ufanje puno radosti, a opakima je nada uprazno.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
Gospodnji je put okrilje bezazlenu, a propast onima koji čine zlo.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Pravednik se neće nikad pokolebati, a opakih će nestati s lica zemlje.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
Pravednikova usta rađaju mudrošću, a opak jezik čupa se s korijenom.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Pravednikove usne znaju što je milo, dok usta opakih poznaju zloću.

< Mithali 10 >