< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
所羅門的箴言: 智慧之子使父親歡樂; 愚昧之子叫母親擔憂。
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
不義之財毫無益處; 惟有公義能救人脫離死亡。
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
耶和華不使義人受飢餓; 惡人所欲的,他必推開。
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
手懶的,要受貧窮; 手勤的,卻要富足。
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
夏天聚斂的,是智慧之子; 收割時沉睡的,是貽羞之子。
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
福祉臨到義人的頭; 強暴蒙蔽惡人的口。
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
義人的紀念被稱讚; 惡人的名字必朽爛。
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
心中智慧的,必受命令; 口裏愚妄的,必致傾倒。
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
行正直路的,步步安穩; 走彎曲道的,必致敗露。
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
以眼傳神的,使人憂患; 口裏愚妄的,必致傾倒。
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
義人的口是生命的泉源; 強暴蒙蔽惡人的口。
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
恨能挑啟爭端; 愛能遮掩一切過錯。
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
明哲人嘴裏有智慧; 無知人背上受刑杖。
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
智慧人積存知識; 愚妄人的口速致敗壞。
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
富戶的財物是他的堅城; 窮人的貧乏是他的敗壞。
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
義人的勤勞致生; 惡人的進項致死。
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
謹守訓誨的,乃在生命的道上; 違棄責備的,便失迷了路。
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
隱藏怨恨的,有說謊的嘴; 口出讒謗的,是愚妄的人。
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
多言多語難免有過; 禁止嘴唇是有智慧。
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
義人的舌乃似高銀; 惡人的心所值無幾。
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
義人的口教養多人; 愚昧人因無知而死亡。
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
耶和華所賜的福使人富足, 並不加上憂慮。
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
愚妄人以行惡為戲耍; 明哲人卻以智慧為樂。
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
惡人所怕的,必臨到他; 義人所願的,必蒙應允。
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
暴風一過,惡人歸於無有; 義人的根基卻是永久。
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
懶惰人叫差他的人 如醋倒牙,如煙薰目。
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
敬畏耶和華使人日子加多; 但惡人的年歲必被減少。
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
義人的盼望必得喜樂; 惡人的指望必致滅沒。
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
耶和華的道是正直人的保障, 卻成了作孽人的敗壞。
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
義人永不挪移; 惡人不得住在地上。
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
義人的口滋生智慧; 乖謬的舌必被割斷。
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
義人的嘴能令人喜悅; 惡人的口說乖謬的話。

< Mithali 10 >