< Wafilipi 1 >

1 Waraka wa Paulo na Timotheo, watumishi wa Kristo Yesu: Kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu walioko Filipi, pamoja na waangalizi na mashemasi:
Bulu mba Timoti igran Yesu, hi bi wa ba ziba ni mi Yesu wa ba he ni Filibi ni biwa ba nji coci ni dikinoni.
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
Ndu zizi he ni yi ni' si Irji tiembu nda tie Bacimbu Yesu Kristi
3 Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.
Mi ngri ni Rji ni nton wa' mi tamre mbia.
4 Katika maombi yangu yote daima nimekuwa nikiwaombea ninyi nyote kwa furaha,
Ko ni tanyi wami tie bre Irji ni yiwu, mi tie bre ni ngryi.
5 kwa sababu ya kushiriki kwenu katika kueneza Injili, tangu siku ya kwanza hadi leo.
Mi ngryi yi wu wa bi wu ta ni to du Rji ni fin umumum'e har ye zizan.
6 Nina hakika kwamba yeye aliyeianza kazi njema mioyoni mwenu, ataiendeleza na kuikamilisha hata siku ya Kristo Yesu.
Mi kpa nyme ni kpi biyi wawu, wawu wa ati tun ndinti ni mi bi arji kle du nra bi ni ye ivri Rji.
7 Ni haki na ni wajibu wangu kufikiri hivi juu yenu nyote, kwa sababu ninyi mko moyoni mwangu. Ikiwa nimefungwa au nikiwa ninaitetea na kuithibitisha Injili, ninyi nyote mnashiriki neema ya Mungu pamoja nami.
Abi na kyi wa mi wo itre ndindi ni tun bi bi he ni sroun mu. Bi yi wawu bi gpo gba mu ni mi dun Rji ni tre ma.
8 Mungu ni shahidi wangu jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote kwa huruma ya Kristo Yesu.
Rji ton sroun mu wa mi hewu niyi ni son wu Kristi ye ni yi
9 Haya ndiyo maombi yangu: kwamba upendo wenu uongezeke zaidi na zaidi katika maarifa na ufahamu wote,
Mi bra ni yi wu dei son bi ndi kwuci ni tre Rji.
10 ili mpate kutambua yale yaliyo mema, mkawe safi, wasio na hatia hadi siku ya Kristo,
In bremu niyiwu dei tsre ndidi ni kon wa abi. Mi bre niyiwu ndi yi tsre gye gyer meni kon Rji.
11 mkiwa mmejawa na matunda ya haki yapatikanayo kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa za Mungu.
Wayi akiyi di Rji ni srendinbi wa Yesu ni nun wa inde Rji ni bi.
12 Basi, ndugu zangu, nataka mjue kwamba mambo yale yaliyonipata kwa kweli yamesaidia sana kueneza Injili.
I mri vayi mi son duyi ton ikpi mba sisre dun ha'ni tre Rji.
13 Matokeo yake ni kwamba imejulikana wazi kwa walinzi wote wa jumba la kifalme na kwa wengine wote kuwa nimefungwa kwa ajili ya Kristo.
Don tre Rji iya si kpa biwa mba sre ni kon Yesu.
14 Kwa sababu ya vifungo vyangu, ndugu wengi katika Bwana wametiwa moyo kuhubiri neno la Mungu kwa ujasiri zaidi na bila woga.
Imri vayi gbugbu mba kri gbangban wa mba to me nimi sara, nda kri gban gban ni zan mba handa tre tre Rji
15 Ni kweli kwamba wengine wanamhubiri Kristo kutokana na wivu na kwa kutaka kushindana, lakini wengine wanamhubiri Kristo kwa nia njema.
Mba ri mba tre tre Rji ni mi fu ni son sroun, mbari ni sroun ndiki.
16 Hawa wa mwisho wanamhubiri Kristo kwa moyo wa upendo, wakifahamu kwamba nimo humu gerezani kwa ajili ya kuitetea Injili.
Bi tre tre Rji ni sroun ndindi mbato mba zi me nde me kle du tre Rji.
17 Hao wa kwanza wanamtangaza Kristo kutokana na tamaa zao wenyewe wala si kwa moyo mweupe, bali wanakusudia kuongeza mateso yangu katika huku kufungwa kwangu.
Mbari mba tre tre Rji dun son tun, ni sroun meme, ni impre mba ndi mba zitrenya ni mi yan.
18 Lakini inadhuru nini? Jambo la muhimu ni kwamba kwa kila njia, ikiwa ni kwa nia mbaya au njema, Kristo anahubiriwa. Nami kwa ajili ya jambo hilo ninafurahi. Naam, nami nitaendelea kufurahi,
Ni kon meme, kon ni meme bi tre tre Yesu, me gri, ra zizan me ngryi.
19 kwa maana ninajua kwamba kwa maombi yenu na kwa msaada unaotolewa na Roho wa Yesu Kristo, yale yaliyonipata mimi yatageuka kuwa wokovu wangu.
Ni kon yi mi gbukbun ni sara. wa ni he wa bi bra nimu, ni zo Ruhu Yesu Kristi.
20 Ninatarajia kwa shauku kubwa na kutumaini kwamba sitaaibika kwa njia yoyote, bali nitakuwa na ujasiri wa kutosha ili sasa kama wakati mwingine wowote, Kristo atukuzwe katika mwili wangu, ikiwa ni kwa kuishi au kwa kufa.
A bra mu ni son mu, mi na sha sha nan ni sroun mu wawu, Yesu son ni sroun mu kon mi ni ri kon kwu.
21 Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
Ndi me he ni re a Kristi, ndi mi kwu a kwuci.
22 Kama nitaendelea kuishi katika mwili, kwangu hili ni kwa ajili ya matunda ya kazi. Lakini sijui nichague lipi? Mimi sijui!
Wa mi tsre ni kpa wa zo me wu tre Rji me ma to wa me huna.
23 Ninavutwa kati ya mambo mawili: Ninatamani kuondoka nikakae pamoja na Kristo, jambo hilo ni bora zaidi.
Ha ri mba ba mba mre mu Mremu ndi bri wirji yi ndi he ni Almasihu wa yi ni fin.
24 Lakini kwa sababu yenu ni muhimu zaidi mimi nikiendelea kuishi katika mwili.
Tsre mu ni kpa alele ni yiwu.
25 Kwa kuwa nina matumaini haya, ninajua kwamba nitaendelea kuwepo na kuwa pamoja nanyi nyote, ili mpate kukua na kuwa na furaha katika imani.
Mi to wa yi alele ani ha na kiyi, wa mi he niyi, ni tse sroun bi, ni mi sroun bi.
26 Ili kwamba furaha yenu iwe nyingi katika Kristo Yesu kwa ajili yangu kwa kule kuja kwangu kwenu tena.
Yagan bi ni mi Almasihu Kristi a ni gji kwui do kba ye ni yi.
27 Lakini lolote litakalotukia, mwenende kama ipasavyo Injili ya Kristo, ili kwamba nikija na kuwaona au ikiwa sipo, nipate kusikia haya juu yenu: Kuwa mnasimama imara katika roho moja, mkiishindania imani ya Injili kwa umoja,
Tsre gyegyer ni kon Rji, ko mi ye komina ye na mi ku wo bi kyi gbegba ni mi enbru ndidi. me gri ndu mi wo ndi bisi tsre gyegyer ni kon Rji.
28 wala msitishwe na wale wanaowapinga. Hii ni ishara kwao kuwa wataangamia, lakini ninyi mtaokolewa, na hii ni kazi ya Mungu.
Na klu sistri biwa mbana son yina. ni mba wu a kwu ni tawu a kon ndurh ma wayi rji ni Rji.
29 Kwa maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, bali pia kuteswa kwa ajili yake,
Mba te didi niwu dun Almasihu ana kpa Almasihu megen na, bi sha ya men.
30 kwa kuwa mnashiriki mashindano yale yale mliyoyaona nikiwa nayo na ambayo hata sasa mnasikia kuwa bado ninayo.
Bizi shaya iri mu wa bi zi to, wa bi zi wo sha yan.

< Wafilipi 1 >