< Wafilipi 4 >

1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
Así que mis hermanos, amados y quien tanto deseo ver, mi alegría y mi corona, sean fuertes en el Señor, mis amados.
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
Pido a Evodia y Síntique que tengan la misma opinión en el Señor.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
Y te pido, fiel ayudante en mi trabajo, que veas las necesidades de aquellas mujeres que participaron conmigo en el mensaje de la salvación, con Clement y el resto de mis compañeros de trabajo cuyos nombres están en el libro de la vida.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
Alégrense en el Señor en todo tiempo; otra vez digo: Alégrense.
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Dejen que su comportamiento amable sea claro para todos los hombres. El Señor está cerca.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
En nada estén afanosos; pero en todo con oración, ruegos y acción de gracias hagan saber sus peticiones ante Dios.
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
Y la paz de Dios, que es más profunda que todo conocimiento, guardará sus corazones y sus mentes en Cristo Jesús.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Por lo demás, mis hermanos, todo lo que es verdadero, todo lo que tiene honor, todo lo que es recto, todo lo que es santo, todo lo que es bello, todo lo que tiene valor, si hay alguna virtud y si hay alguna alabanza, piensa en estas cosas.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Las cosas que aprendieron por mi enseñanza y mi predicación, y que viste en mí, estas cosas hagan, y el Dios de paz estará con ustedes.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
Pero estoy muy contento en el Señor porque ustedes han vuelto a pensar en mí; aunque de hecho pensaron en mí, pero no tuvieron oportunidad de ayudarme.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
Pero no lo digo porque tenga necesidad, porque puedo, donde sea que esté, depender de mí mismo.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
Es lo mismo para mí si soy menospreciado u honrado; en todas partes y en todas las cosas, tengo el secreto de cómo estar lleno y cómo ir sin comida; como tener riqueza y cómo estar en necesidad.
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Puedo hacer todas las cosas por medio de aquel que me fortalece.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Pero hiciste bien en cuidarme en mi necesidad.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
Y saben, Filipenses, que cuando les llegó la predicación del evangelio, cuando me fui de Macedonia, ninguna iglesia participó conmigo en él dar y recibir a los santos, sino solo ustedes;
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
Porque incluso en Tesalónica me enviaron una y otra vez en mi necesidad.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
No es que busque una ofrenda, sino un fruto que pueda acreditarse a su cuenta.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
Tengo todo y más que suficiente: estoy lleno, habiendo recibido de Epafrodito lo que vino de ustedes un perfume de olor dulce, una ofrenda que agrada a Dios.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
Y mi Dios les dará todo lo que necesitan de la riqueza de su gloria en Cristo Jesús.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
Ahora a Dios nuestro Padre sea la gloria por los siglos de los siglos. Que así sea. (aiōn g165)
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Dale saludos a cada santo en Cristo Jesús. Los hermanos que están conmigo les envían saludos.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
Todos los santos les envían saludos, especialmente los que son de la casa del César.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
La gracia del Señor Jesucristo sea con ustedes.

< Wafilipi 4 >