< Wafilipi 4 >

1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
Por tanto, hermanos míos, amados y anhelados, mi alegría y mi corona, manteneos firmes en el Señor de esta manera, amados míos.
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
Exhorto a Euodia, y exhorto a Syntyche, a que piensen de la misma manera en el Señor.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
Sí, te ruego también a ti, compañero verdadero, que ayudes a estas mujeres, pues ellas trabajaron conmigo en la Buena Nueva, con Clemente también, y con los demás colaboradores míos, cuyos nombres están en el libro de la vida.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
¡Alégrense siempre en el Señor! De nuevo diré: “¡Alégrense!”
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Que tu mansedumbre sea conocida por todos los hombres. El Señor está cerca.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
En nada os afanéis, sino que en todo, mediante la oración y la petición con acción de gracias, presentad vuestras peticiones a Dios.
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
Y la paz de Dios, que sobrepasa todo entendimiento, guardará vuestros corazones y vuestros pensamientos en Cristo Jesús.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Por último, hermanos, todo lo que es verdadero, todo lo que es honorable, todo lo que es justo, todo lo que es puro, todo lo que es hermoso, todo lo que es de buena reputación: si hay alguna virtud y si hay algo digno de alabanza, pensad en estas cosas.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Haced lo que habéis aprendido, recibido, oído y visto en mí, y el Dios de la paz estará con vosotros.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
Pero me regocijo mucho en el Señor de que ahora, por fin, hayas revivido tu pensamiento por mí, en el que sí pensabas, pero te faltaba la oportunidad.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
No es que hable por falta, pues he aprendido a contentarme en cualquier estado en que me encuentre.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
Sé cómo ser humilde, y también sé cómo abundar. En todas y cada una de las circunstancias he aprendido el secreto tanto de estar saciado como de tener hambre, tanto de abundar como de estar necesitado.
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Todo lo puedo en Cristo, que me fortalece.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Sin embargo, habéis hecho bien en participar en mi aflicción.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
Vosotros mismos sabéis también, filipenses, que al principio de la Buena Nueva, cuando partí de Macedonia, ninguna asamblea compartía conmigo el dar y el recibir, sino sólo vosotros.
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
Pues incluso en Tesalónica enviasteis una y otra vez a mi necesidad.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
No es que busque el don, sino que busco el fruto que aumenta a vuestra cuenta.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
Pero yo lo tengo todo y me sobra. Estoy lleno, habiendo recibido de Epafrodito las cosas que vinieron de ti, una fragancia agradable, un sacrificio aceptable y agradable a Dios.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
Mi Dios suplirá toda necesidad tuya según sus riquezas de gloria en Cristo Jesús.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
Al Dios y Padre nuestro sea la gloria por los siglos de los siglos. Amén. (aiōn g165)
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Saludad a todos los santos en Cristo Jesús. Los hermanos que están conmigo os saludan.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
Os saludan todos los santos, especialmente los de la casa del César.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
La gracia del Señor Jesucristo esté con todos vosotros. Amén.

< Wafilipi 4 >