< Wafilipi 4 >
1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
Przetoż, bracia moi mili i pożądani! radości i korono moja! tak stójcie w Panu, najmilsi moi!
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
Ewodyi proszę i Syntychy proszę, aby jednegoż rozumienia były w Panu.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
Proszę też i cię, towarzyszu wierny! bądź tym na pomoc, które w Ewangielii wespół ze mną pracowały, i z Klemensem i z innymi pomocnikami moimi, których imiona są w księgach żywota.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
Radujcie się zawsze w Panu; znowu mówię, radujcie się.
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Skromność wasza niech będzie wiadoma wszystkim ludziom; Pan blisko jest.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Nie troszczcie się o żadną rzecz, ale we wszystkiem przez modlitwę i prośbę z dziękowaniem żądności wasze niech będą znajome u Boga.
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
A pokój Boży, który przewyższa wszelki rozum, będzie strzegł serc waszych i myśli waszych w Chrystusie Jezusie.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
A dalej mówiąc, bracia, cokolwiek jest prawdziwego, cokolwiek poczciwego, cokolwiek sprawiedliwego, cokolwiek czystego, cokolwiek przyjemnego, cokolwiek chwalebnego, jeźli która cnota i jeźli która chwała, o tem przemyślajcie.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Czegoście się też nauczyli i coście przyjęli, i słyszeli, i widzieli przy mnie, to czyńcie, a Bóg pokoju będzie z wami.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
A uradowałem się wielce w Panu, żeście się już wżdy znowu zazielenili w swojem staraniu o mię, jakoż i staraliście się o to, lecz wam na sposobnym czasie schodziło.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
Nie żebym to mówił dla niedostatku; bomci się ja nauczył, na tem przestawać, co mam.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
Umiem i uniżać się, umiem i obfitować; wszędy i we wszystkich rzeczach jestem wyćwiczony i nasyconym być, i łaknąć, i obfitować, i niedostatek cierpieć;
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Wszystko mogę w Chrystusie, który mię posila.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Wszakże dobrzeście uczynili, żeście społecznie dogodzili uciskowi mojemu.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
A wiecie i wy Filipensowie, iż na początku Ewangielii, gdym wyszedł z Macedonii, żaden mi zbór nie udzielił na rachunek dawania i brania, tylko wy sami;
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
Ponieważ i do Tesaloniki raz i drugi, czego potrzeba było, posłaliście mi,
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
Nie przeto, żebym datku szukał; ale szukam pożytku, który by obfitował na rachunku waszym.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
Gdyżem odebrał wszystko i mam dostatek, pełenem, wziąwszy od Epafrodyta, co posłano od was, wonność dobrego zapachu, ofiarę przyjemną i Bogu się podobającą.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
A Bóg mój napełni wszelką potrzebę waszę według bogactwa swego, chwalebnie, w Chrystusie Jezusie.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
A Bogu i Ojcu naszemu niech będzie chwała na wieki wieków. Amen. (aiōn )
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Pozdrówcie wszystkich świętych w Chrystusie Jezusie. Pozdrawiają was bracia, którzy są ze mną.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
Pozdrawiają was wszyscy święci; ale osobliwie, którzy są z cesarskiego domu.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
Łaska Pana naszego Jezusa Chrystusa niech będzie z wami wszystkimi. Amen.