< Wafilipi 4 >
1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
C’est pourquoi, mes frères très chers et très désirés, ma gloire et ma couronne, demeurez ainsi fermes dans le Seigneur, mes bien-aimés,
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
Je prie Evodie et je conjure Syntyche d’avoir les mêmes sentiments dans le Seigneur.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
Je te prie aussi, toi, mon fidèle compagnon, aide celles qui ont travaillé avec moi pour l’Evangile, avec Clément et mes autres coopérateurs, dont les noms sont dans le livre de vie.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
Réjouissez-vous toujours dans le Seigneur; je le dis encore, réjouissez-vous.
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Que votre modestie soit connue de tous les hommes; le Seigneur est proche.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Ne vous inquiétez de rien, mais que dans toutes vos prières et dans toutes vos supplications ce soit avec des actions de grâces que vos demandes paraissent devant Dieu.
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
Et que la paix de Dieu, qui surpasse toute pensée, garde vos cœurs et vos esprits dans le Christ Jésus.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Enfin, mes frères, que tout ce qui est vrai, tout ce qui est pur, tout ce qui est juste, tout ce qui est saint, tout ce qui est aimable, toute bonne réputation, tout ce qui est vertueux, tout ce qui est louable dans les mœurs, soit l’objet de vos pensées.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Ce que vous avez appris, et reçu, et entendu de moi, et vu en moi, pratiquez-le, et le Dieu de paix sera avec vous.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
Au reste, je me suis grandement réjoui dans le Seigneur de ce que vos sentiments pour moi ont enfin refleuri: vous les aviez toujours, mais vous étiez occupés.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
Ce n’est pas à cause du besoin que j’en ai que je parle ainsi; car j’ai appris à être satisfait de l’état où je me trouve.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
Je sais être humilié, et je sais aussi vivre dans l’abondance (je me suis habitué partout et à tout); être rassasié et avoir faim; être dans l’abondance et dans l’indigence.
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Je puis tout en celui qui me fortifie.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Cependant vous avez bien fait en prenant part à mes tribulations.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
Or vous savez, vous aussi, Philippiens, qu’au commencement de ma prédication de l’Evangile, quand je partis de la Macédoine, aucune Eglise ne m’a fait part de ses biens à titre de compensation, si ce n’est vous seuls;
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
Car vous m’avez envoyé une fois, et même deux, à Thessalonique, ce qui m’était nécessaire.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
Non que je recherche vos dons, mais je désire le fruit qui en abondera par rapport à vous.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
Car j’ai tout, j’abonde; je suis comblé, ayant reçu par Epaphrodite ce que vous avez envoyé, oblation de suave odeur, hostie acceptée, agréable à Dieu.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
Mais que mon Dieu remplisse tous vos désirs, selon ses richesses en gloire, dans le Christ Jésus.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
À Dieu notre Père, gloire dans tous les siècles. Amen. (aiōn )
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Saluez tous les saints en Jésus-Christ.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
Les frères qui sont avec moi vous saluent. Tous les saints vous saluent, mais principalement ceux qui sont de la maison de César.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
Que la grâce de Notre Seigneur Jésus-Christ soit avec votre esprit. Amen.