< Wafilipi 4 >
1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
Therefore, my brethren dearly beloved and longed for, my joy and crown, so stand fast in the Lord, [my] dearly beloved.
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
I beseech Euodias, and beseech Syntyche, that they be of the same mind in the Lord.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
And I entreat thee also, true yoke-fellow, help those women who labored with me in the gospel, with Clement also, and [with] other my fellow-laborers, whose names [are] in the book of life.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
Rejoice in the Lord always: [and] again I say, Rejoice.
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Let your moderation be known to all men. The Lord [is] at hand.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Be anxious for nothing; but in every thing by prayer and supplication with thanksgiving let your requests be made known to God.
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
And the peace of God, which passeth all understanding, will keep your hearts and minds through Christ Jesus.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Finally, brethren, whatever things are true, whatever things [are] honest, whatever things [are] just, whatever things [are] pure, whatever things [are] lovely, whatever things [are] of good report; if [there is] any virtue, and if [there is] any praise, think on these things.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Those things, which ye have both learned, and received, and heard, and seen in me, do: and the God of peace will be with you.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
But I rejoiced in the Lord greatly, that now at the last your care of me hath flourished again; wherein ye were also careful, but ye lacked opportunity.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
Not that I speak in respect of want: for I have learned, in whatever state I am, [with that] to be content.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
I know both how to be abased, and I know how to abound: every where and in all things I am instructed both to be full and to be hungry, both to abound and to suffer need.
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
I can do all things through Christ who strengtheneth me.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Notwithstanding ye have done well, that ye did communicate with my affliction.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
Now, ye Philippians, know also, that in the beginning of the gospel, when I departed from Macedonia, no church communicated with me as concerning giving and receiving, but ye only.
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
For even in Thessalonica ye sent once and again to my necessity.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
Not because I desire a gift: but I desire fruit that may abound to your account.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
But I have all, and abound: I am full, having received from Epaphroditus the things [which were sent] from you, an odor of a sweet smell, a sacrifice acceptable, well-pleasing to God.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
But my God will supply all your need according to his riches in glory by Christ Jesus.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
Now to God and our Father [be] glory for ever and ever. Amen. (aiōn )
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Salute every saint in Christ Jesus. The brethren who are with me greet you.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
All the saints salute you, chiefly they that are of Cesar's household.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ [be] with you all. Amen.