< Wafilipi 4 >
1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
Therefore, my beloved brothers whom I long for, my joy and crown, in this way stand firm in the Lord, beloved friends.
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
I am pleading with Euodia, and I am pleading with Syntyche, be of the same mind in the Lord.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
Yes, I ask you, my true companion, to help these women who labored with me in spreading the gospel, along with Clement and the rest of my fellow workers, whose names are in the Book of Life.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
Rejoice in the Lord always. Again I will say, rejoice.
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Let your gentleness be known to all people. The Lord is near.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Do not be anxious about anything. Instead, in everything by prayer and petition with thanksgiving, let your requests be known to God,
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
and the peace of God, which surpasses all understanding, will guard your hearts and your thoughts in Christ Jesus.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Finally, brothers, whatever things are true, whatever things are honorable, whatever things are just, whatever things are pure, whatever things are lovely, whatever things are of good report, if there is anything excellent, if there is anything to be praised, think about these things.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
The things that you have learned and received and heard and seen in me, do these things, and the God of peace will be with you.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
I greatly rejoice in the Lord because now at last you have renewed your concern for me. You had indeed been concerned for me before, but there was no opportunity for you to help.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
I am not saying this because I am in need. For I have learned to be content in all circumstances.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
I know what it is to be poor, and I also know what it is to have plenty. In every way and in all things I have learned the secret of how to be well-fed or to be hungry, and how to have an abundance or to be in need.
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
I can do all things through him who strengthens me.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
However, you did well to share with me in my difficulties.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
You Philippians know that in the beginning of the gospel, when I left Macedonia, no church supported me in the matter of giving and receiving except you alone.
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
Even when I was in Thessalonica, you sent help for my needs more than once.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
It is not that I seek the gift. Instead, I seek the fruit that increases to your credit.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
I have received everything in full, and even more. I have been well-supplied now that I have received from Epaphroditus the things you sent. They are a sweet-smelling aroma, a sacrifice acceptable and pleasing to God.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
My God will meet all your needs according to his riches in glory in Christ Jesus.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
Now to our God and Father be the glory forever and ever. Amen. (aiōn )
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Greet every believer in Christ Jesus. The brothers who are with me greet you.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
All the believers here greet you, especially those of Caesar's household.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
May the grace of the Lord Jesus Christ be with your spirit.