< Wafilipi 4 >
1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
My fellow believers, I love you, and I long for you. You make me happy [MTY], and I am (proud of/pleased with) you. Dear friends, on the basis [of all that I have told you], continue to believe firmly in the Lord doing what I have just taught you.
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
I urge [you(sg)], Euodia, and I urge [you(sg)], Syntyche, to again have a peaceful relationship with each other, [because you both have a relationship with] the Lord.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
And, my faithful comrade/partner, I request that you [(sg)] help them [to again have a peaceful relationship with each other], because they have [faithfully proclaimed] the message [about Christ] together with me, [even though many people] have opposed us [(exc)]. They have faithfully proclaimed that message together with Clement and the rest of my fellow workers, whose names [are] in the book [in which God has written the names of all those people who will] live [forever].
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
[Because you have a relationship with] the Lord, always rejoice! I’m saying it again, rejoice!
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
[Act in such a way that] everyone can know that you are gentle. The Lord is coming soon.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Do not worry about anything. Instead, in every situation, pray [to God], tell him what you need, and ask him [to help you] [DOU]. Also thank [him for what he does for you].
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
As a result, God will enable you not to worry [about anything] [MTY] (OR, God will protect your minds [in every way]) [PRS]. [That is], he will cause you to have [inner] peace [because you have a relationship with] Christ Jesus. You will not be able to understand [PRS] [how you can be so peaceful in such difficult circumstances!]!
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
My fellow believers, there is one more thing I [want you to do]. Whatever is true, whatever is worthy of respect, whatever is right, whatever is morally pure, whatever is pleasing, whatever is admirable, whatever is good, whatever [deserves] praise, those are the things that you should continually think about.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Those things that I have taught you and that you have learned from me, those things that you have heard me [say] and that you have seen me [do], those are the things that you yourselves should continually do. As a result [of your doing those things], God, the one who [causes us to] have [inner] peace, will (be with/bless) you.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
I rejoice greatly [and thank] the Lord because now, after some time, [by sending money to me] you have once again shown that you are concerned about me [EUP]. Indeed, you were concerned about me [all the time], but you had no opportunity [to show that you were concerned about me].
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
I am saying this not because I [am concerned that I] lack things [that I need]. In fact, I have learned to be content in whatever [situation] I am.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
[Specifically], I know how [to be content when] I do not have what I need, and I know how [to be content when] I have plenty. I have learned how [to be content] in any and every [situation] [DOU]. [Specifically], I have learned how [to be content when] I have enough to eat, and I have learned how [to be content when] I do not have enough to eat. I have learned how [to be content when] I have plenty [DOU] [of what I need], and I have learned [how to be content when] I lack [things].
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
I am able (to cope with/to handle) every situation because [Christ] gives me the strength to do that.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Nevertheless, you did very well by [helping me] (OR, [giving me money]) [EUP] while I have been suffering hardship.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
[My friends there at Philippi], you yourselves know that when I first [proclaimed] the message about Christ [to you], and then left there to go to Macedonia [province], you were the only group of believers [LIT] who [sent me] gifts [EUP] in order that I might [proclaim that message] to others just like I did for you.
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
Even [when I was] in Thessalonica [city], you sent [money] [EUP] to me two different times [IDM] in order to [supply] what I needed.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
I say this, not because I desire that you give me money now. Instead, I desire that [God] will abundantly bless [MET] you as a result of [your helping me].
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
But I have received a very generous [gift] [EUP] [from you], and [as a result], I have plenty. I have an abundant supply [of what I need because] I have received from Epaphroditus the money [EUP] that you [sent to me]. God considers that your gift is very acceptable, and he is very pleased with it. [Your gift is like] a nice-smelling sacrifice [MET].
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
[Moreover], God, [whom] I [serve], has an unlimited supply [of everything that we(inc) need]. And as a result, because of your relationship with Christ Jesus, he will completely supply everything that you need.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
[So], praise God our Father forever and ever! Amen! (aiōn )
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Greet [for me/us(exc)] all of God’s people [there, that is, all those who have a relationship with] Christ Jesus. The fellow believers who [serve God together] with me here send their greetings to you (OR, say they are thinking fondly of you).
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
All of God’s people [here] send their greetings to you. Especially the [fellow believers who work] in the palace of the emperor send their greetings to you.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
My desire is [that our] Lord Jesus Christ [will continue to] act kindly toward you all [SYN].