< Wafilipi 4 >
1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
So then, my dear friends, whom I am longing to see – you who are my joy and my crown, stand fast in union with the Lord, dear friends.
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
I entreat Euodia, and I entreat Syntyche, to live in harmony, in union with the Lord;
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
yes, and I ask you, my true comrade, to help them, remembering that they toiled by my side in spreading the good news; and so, too, did Clement and my other fellow workers, whose names are in the book of life.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
All joy be yours at all times in your union with the Lord. Again I repeat – All joy be yours.
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Let your forbearing spirit be plain to everyone. The Lord is near.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Do not be anxious about anything; but under all circumstances, by prayer and entreaty joined with thanksgiving, make your needs known to God.
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
Then the peace of God, which is beyond all human understanding, will stand guard over your hearts and thoughts, through your union with Christ Jesus.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
In conclusion, friends, whenever you find things that are true or honorable, righteous or pure, lovable or praiseworthy, or if virtue and honor have any meaning, let them fill your thoughts.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
All that you learned and received and heard and saw in me put into practice continually; and then God, the giver of peace, will be with you.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
It was a matter of great joy to me, as one in union with the Lord, that at length your interest in me had revived. The interest indeed you had, but not the opportunity.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
Do not think that I am saying this under the pressure of want. For I, however I am placed, have learned to be independent of circumstances.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
I know how to face humble circumstances, and I know how to face prosperity. Into all and every human experience I have been initiated – into plenty and hunger, into prosperity and want.
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
I can do everything through the strength of the one who makes me strong!
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Yet you have acted nobly in sharing my troubles.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
And you at Philippi know, as well as I, that in the early days of the good news – at the time when I had just left Macedonia – no church, with the one exception of yourselves, had anything to do with me as far as giving and receiving are concerned.
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
Indeed, even while I was still in Thessalonica, you sent more than once to relieve my wants.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
It is not that I am anxious for your gifts, but I am anxious to see the abundant return that will be placed to your account. I have enough of everything, and to spare.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
My wants are fully satisfied, now that I have received from Epaphroditus the gifts which you sent me – the sweet fragrance of a sacrifice acceptable and pleasing to God.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
And my God, out of the greatness of his wealth, will, in glory, fully satisfy your every need, through your union with Christ Jesus.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn )
To him, our God and Father, be ascribed all glory for every and ever. Amen. (aiōn )
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Give my greeting to everyone of the people of Christ Jesus. The Lord’s followers who are with me send your their greetings.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
All Christ’s people here, and especially those who belong to the Emperor’s household, send theirs.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
May the blessing of the Lord Jesus Christ rest on your souls.