< Wafilipi 4 >

1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
Derfor, mine Brødre, elskede og savnede, min Glæde og Krans! staar saaledes fast i Herren, I elskede!
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
Evodia formaner jeg, og Syntyke formaner jeg til at være enige i Herren.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
Ja, jeg beder ogsaa dig, min ægte Synzygus! tag dig af dem; thi de have med mig stridt i Evangeliet, tillige med Klemens og mine øvrige Medarbejdere, hvis Navne staa i Livets Bog.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
Glæder eder i Herren altid; atter siger jeg: Glæder eder!
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Eders milde Sind vorde kendt af alle Mennesker! Herren er nær!
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Værer ikke bekymrede for noget, men lader i alle Ting eders Begæringer komme frem for Gud i Paakaldelse og Bøn med Taksigelse;
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
og Guds Fred, som overgaar al Forstand, skal bevare eders Hjerter og eders Tanker i Kristus Jesus.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
I øvrigt, Brødre! alt, hvad der er sandt, hvad der er ærbart, hvad der er retfærdigt, hvad der er rent, hvad der er elskeligt, hvad der har godt Lov, enhver Dyd og enhver Hæder: Lægger eder det paa Sinde!
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
Hvad I baade have lært og modtaget og hørt og set paa mig, dette skulle I gøre, og Fredens Gud skal være med eder.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
Men jeg har højlig glædet niig i Herren over, at I nu omsider ere komne til Kræfter, saa at I kunne tænke paa mit Vel, hvorpaa I ogsaa forhen tænkte, men I manglede Lejlighed.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
Dette siger jeg ikke af Trang; thi jeg har lært at nøjes med det, jeg har.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
Jeg forstaar at være i ringe Kaar, og jeg forstaar ogsaa at have Overflod; i alt og hvert er jeg indviet, baade i at mættes og i at hungre, baade i at have Overflod og i at lide Savn.
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Alt formaar jeg i ham, som gør mig stærk.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Dog gjorde I vel i at tage Del i min Trængsel.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
Men I vide det ogsaa selv, Filippensere! at i Evangeliets Begyndelse, da jeg drog ud fra Makedonien, var der ingen Menighed, som havde Regning med mig over givet og modtaget, uden I alene.
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
Thi endog i Thessalonika sendte I mig baade en og to Gange, hvad jeg havde nødig.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
Ikke at jeg attraar Gaven, men jeg attraar den Frugt, som bliver rigelig til eders Fordel.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
Nu har jeg nok af alt og har Overflod; jeg har fuldt op efter ved Epafroditus at have modtaget eders Gave, en Vellugts-Duft, et velkomment Offer, velbehageligt for Gud.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
Men min Gud skal efter sin Rigdom fuldelig give eder alt, hvad I have nødig, i Herlighed i Kristus Jesus.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
Men ham, vor Gud og Fader, være Æren i Evigheders Evigheder! Amen. (aiōn g165)
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
Hilser hver hellig i Kristus Jesus.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
De Brødre, som ere hos mig, hilse eder. Alle de hellige hilse eder, men mest de af Kejserens Hus.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
Den Herres Jesu Kristi Naade være med eders Aand!

< Wafilipi 4 >