< Wafilipi 3 >

1 Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana! Mimi kuwaandikia mambo yale yale hakuniudhi, kwa maana ni kinga kwa ajili yenu.
W końcu, moi bracia, radujcie się w Panu. Pisać do was o tym samym mnie nie męczy, a dla was [jest] bezpieczne.
2 Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa.
Strzeżcie się psów, strzeżcie się złych pracowników, strzeżcie się obrzezywaczy.
3 Kwa maana sisi ndio tulio tohara, sisi tumwabuduo Mungu katika Roho, tunaona fahari katika Kristo Yesu, ambao hatuweki tumaini letu katika mwili,
My bowiem jesteśmy obrzezaniem, którzy w duchu służymy Bogu i chlubimy się w Chrystusie Jezusie, a nie pokładamy ufności w ciele.
4 ingawa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuutumainia mwili. Kama mtu yeyote akidhani anazo sababu za kuutumainia mwili, mimi zaidi.
Chociaż i ja mógłbym pokładać ufność w ciele. Jeśli ktoś inny uważa, że może pokładać ufność w ciele, bardziej ja:
5 Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania. Kwa habari ya sheria, ni Farisayo,
Obrzezany ósmego dnia, z rodu Izraela, z pokolenia Beniamina, Hebrajczyk z Hebrajczyków, co do prawa – faryzeusz;
6 kwa habari ya juhudi, nilikuwa nalitesa kanisa, kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria, mimi nilikuwa sina hatia.
Co do gorliwości – prześladowca kościoła, co do sprawiedliwości opartej na prawie – nienaganny.
7 Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
Lecz to, co było dla mnie zyskiem, ze względu na Chrystusa uznałem za stratę.
8 Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo.
Owszem, wszystko uznaję za stratę dla znakomitości poznania Chrystusa Jezusa, mojego Pana, dla którego wszystko utraciłem i uznaję to za gnój, aby zyskać Chrystusa;
9 Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani.
I znaleźć się w nim, nie mając własnej sprawiedliwości, tej, która jest z prawa, ale tę, która jest przez wiarę Chrystusa, [to jest] sprawiedliwość z Boga przez wiarę;
10 Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake,
Żeby poznać jego i moc jego zmartwychwstania oraz [swój] udział w jego cierpieniach, upodabniając się do jego śmierci;
11 ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.
Abym jakimkolwiek sposobem dostąpił powstania z martwych.
12 Si kwamba nimekwisha kufikia, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha! Bali nakaza mwendo ili nipate kile ambacho kwa ajili yake, nimeshikwa na Kristo Yesu.
Nie żebym [to] już osiągnął albo już był doskonały, ale dążę, aby pochwycić to, do czego też zostałem pochwycony przez Chrystusa Jezusa.
13 Ndugu zangu, sijihesabu kuwa nimekwisha kushika. Lakini ninafanya jambo moja: Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele.
Bracia, ja o sobie nie myślę, że już pochwyciłem. Lecz jedno [czynię]: zapominając o tym, co za mną, a zdążając do tego, co przede mną;
14 Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.
Biegnę do mety, do nagrody powołania Bożego, które jest z góry w Chrystusie Jezusie.
15 Hivyo sisi sote tuliokuwa kiroho tuwaze jambo hili, hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu ataliweka wazi hilo nalo.
Ilu więc [nas] jest doskonałych, tak myślmy. A jeśli o czymś inaczej myślicie, i to wam Bóg objawi.
16 Lakini na tushike sana lile ambalo tumekwisha kulifikia.
Jednak [w tym], do czego doszliśmy, postępujmy według jednej miary i to samo myślmy.
17 Ndugu zangu, kwa pamoja fuateni mfano wangu na kuwatazama wale wanaofuata kielelezo tulichowawekea.
Bądźcie, bracia, [wszyscy] razem moimi naśladowcami i przypatrujcie się tym, którzy postępują według wzoru, jaki w nas macie.
18 Kwa maana, kama nilivyokwisha kuwaambia mara nyingi kabla, nami sasa nasema tena hata kwa machozi, watu wengi wanaishi kama adui wa msalaba wa Kristo.
Wielu bowiem, o których wam często mówiłem, postępuje [inaczej], a teraz nawet z płaczem mówię, że są wrogami krzyża Chrystusa.
19 Mwisho wa watu hao ni maangamizi, Mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu, na mawazo yao yamo katika mambo ya dunia.
Ich końcem [jest] zatracenie, ich Bogiem jest brzuch, a ich chwała jest w hańbie; myślą oni o tym, co ziemskie.
20 Lakini uenyeji wetu uko mbinguni. Nasi tunamngoja kwa shauku Mwokozi kutoka huko, yaani, Bwana Yesu Kristo,
Nasza zaś ojczyzna jest w niebie, skąd też oczekujemy Zbawiciela, Pana Jezusa Chrystusa.
21 atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, ili upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote chini yake.
On przemieni nasze podłe ciało, aby było podobne do jego chwalebnego ciała, zgodnie ze skuteczną mocą, którą też może poddać sobie wszystko.

< Wafilipi 3 >