< Wafilipi 1 >
1 Waraka wa Paulo na Timotheo, watumishi wa Kristo Yesu: Kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu walioko Filipi, pamoja na waangalizi na mashemasi:
Paul and Timothy, servants of Christ Jesus, to all the saints in Christ Jesus which are at Philippi, with the bishops and deacons:
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ.
3 Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.
I thank my God upon all my remembrance of you,
4 Katika maombi yangu yote daima nimekuwa nikiwaombea ninyi nyote kwa furaha,
always in every supplication of mine on behalf of you all making my supplication with joy,
5 kwa sababu ya kushiriki kwenu katika kueneza Injili, tangu siku ya kwanza hadi leo.
for your fellowship in furtherance of the gospel from the first day until now;
6 Nina hakika kwamba yeye aliyeianza kazi njema mioyoni mwenu, ataiendeleza na kuikamilisha hata siku ya Kristo Yesu.
being confident of this very thing, that he which began a good work in you will perfect it until the day of Jesus Christ:
7 Ni haki na ni wajibu wangu kufikiri hivi juu yenu nyote, kwa sababu ninyi mko moyoni mwangu. Ikiwa nimefungwa au nikiwa ninaitetea na kuithibitisha Injili, ninyi nyote mnashiriki neema ya Mungu pamoja nami.
even as it is right for me to be thus minded on behalf of you all, because I have you in my heart, inasmuch as, both in my bonds and in the defence and confirmation of the gospel, ye all are partakers with me of grace.
8 Mungu ni shahidi wangu jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote kwa huruma ya Kristo Yesu.
For God is my witness, how I long after you all in the tender mercies of Christ Jesus.
9 Haya ndiyo maombi yangu: kwamba upendo wenu uongezeke zaidi na zaidi katika maarifa na ufahamu wote,
And this I pray, that your love may abound yet more and more in knowledge and all discernment;
10 ili mpate kutambua yale yaliyo mema, mkawe safi, wasio na hatia hadi siku ya Kristo,
so that ye may approve the things that are excellent; that ye may be sincere and void of offence unto the day of Christ;
11 mkiwa mmejawa na matunda ya haki yapatikanayo kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa za Mungu.
being filled with the fruits of righteousness, which are through Jesus Christ, unto the glory and praise of God.
12 Basi, ndugu zangu, nataka mjue kwamba mambo yale yaliyonipata kwa kweli yamesaidia sana kueneza Injili.
Now I would have you know, brethren, that the things [which happened] unto me have fallen out rather unto the progress of the gospel;
13 Matokeo yake ni kwamba imejulikana wazi kwa walinzi wote wa jumba la kifalme na kwa wengine wote kuwa nimefungwa kwa ajili ya Kristo.
so that my bonds became manifest in Christ throughout the whole praetorian guard, and to all the rest;
14 Kwa sababu ya vifungo vyangu, ndugu wengi katika Bwana wametiwa moyo kuhubiri neno la Mungu kwa ujasiri zaidi na bila woga.
and that most of the brethren in the Lord, being confident through my bonds, are more abundantly bold to speak the word of God without fear.
15 Ni kweli kwamba wengine wanamhubiri Kristo kutokana na wivu na kwa kutaka kushindana, lakini wengine wanamhubiri Kristo kwa nia njema.
Some indeed preach Christ even of envy and strife; and some also of good will:
16 Hawa wa mwisho wanamhubiri Kristo kwa moyo wa upendo, wakifahamu kwamba nimo humu gerezani kwa ajili ya kuitetea Injili.
the one [do it] of love, knowing that I am set for the defence of the gospel:
17 Hao wa kwanza wanamtangaza Kristo kutokana na tamaa zao wenyewe wala si kwa moyo mweupe, bali wanakusudia kuongeza mateso yangu katika huku kufungwa kwangu.
but the other proclaim Christ of faction, not sincerely, thinking to raise up affliction for me in my bonds.
18 Lakini inadhuru nini? Jambo la muhimu ni kwamba kwa kila njia, ikiwa ni kwa nia mbaya au njema, Kristo anahubiriwa. Nami kwa ajili ya jambo hilo ninafurahi. Naam, nami nitaendelea kufurahi,
What then? only that in every way, whether in pretence or in truth, Christ is proclaimed; and therein I rejoice, yea, and will rejoice.
19 kwa maana ninajua kwamba kwa maombi yenu na kwa msaada unaotolewa na Roho wa Yesu Kristo, yale yaliyonipata mimi yatageuka kuwa wokovu wangu.
For I know that this shall turn to my salvation, through your supplication and the supply of the Spirit of Jesus Christ,
20 Ninatarajia kwa shauku kubwa na kutumaini kwamba sitaaibika kwa njia yoyote, bali nitakuwa na ujasiri wa kutosha ili sasa kama wakati mwingine wowote, Kristo atukuzwe katika mwili wangu, ikiwa ni kwa kuishi au kwa kufa.
according to my earnest expectation and hope, that in nothing shall I be put to shame, but [that] with all boldness, as always, [so] now also Christ shall be magnified in my body, whether by life, or by death.
21 Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
For to me to live is Christ, and to die is gain.
22 Kama nitaendelea kuishi katika mwili, kwangu hili ni kwa ajili ya matunda ya kazi. Lakini sijui nichague lipi? Mimi sijui!
But if to live in the flesh, —[if] this is the fruit of my work, then what I shall choose I wot not.
23 Ninavutwa kati ya mambo mawili: Ninatamani kuondoka nikakae pamoja na Kristo, jambo hilo ni bora zaidi.
But I am in a strait betwixt the two, having the desire to depart and be with Christ; for it is very far better:
24 Lakini kwa sababu yenu ni muhimu zaidi mimi nikiendelea kuishi katika mwili.
yet to abide in the flesh is more needful for your sake.
25 Kwa kuwa nina matumaini haya, ninajua kwamba nitaendelea kuwepo na kuwa pamoja nanyi nyote, ili mpate kukua na kuwa na furaha katika imani.
And having this confidence, I know that I shall abide, yea, and abide with you all, for your progress and joy in the faith;
26 Ili kwamba furaha yenu iwe nyingi katika Kristo Yesu kwa ajili yangu kwa kule kuja kwangu kwenu tena.
that your glorying may abound in Christ Jesus in me through my presence with you again.
27 Lakini lolote litakalotukia, mwenende kama ipasavyo Injili ya Kristo, ili kwamba nikija na kuwaona au ikiwa sipo, nipate kusikia haya juu yenu: Kuwa mnasimama imara katika roho moja, mkiishindania imani ya Injili kwa umoja,
Only let your manner of life be worthy of the gospel of Christ: that, whether I come and see you or be absent, I may hear of your state, that ye stand fast in one spirit, with one soul striving for the faith of the gospel;
28 wala msitishwe na wale wanaowapinga. Hii ni ishara kwao kuwa wataangamia, lakini ninyi mtaokolewa, na hii ni kazi ya Mungu.
and in nothing affrighted by the adversaries: which is for them an evident token of perdition, but of your salvation, and that from God;
29 Kwa maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, bali pia kuteswa kwa ajili yake,
because to you it hath been granted in the behalf of Christ, not only to believe on him, but also to suffer in his behalf:
30 kwa kuwa mnashiriki mashindano yale yale mliyoyaona nikiwa nayo na ambayo hata sasa mnasikia kuwa bado ninayo.
having the same conflict which ye saw in me, and now hear to be in me.