< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
La vision d'Abdias. Voici ce que dit le Seigneur Yahvé au sujet d'Édom. Nous avons entendu des nouvelles de Yahvé, et un ambassadeur est envoyé parmi les nations, disant: « Levez-vous, et levons-nous contre elle dans la bataille.
2 “Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
Voici, je t'ai rendu petit parmi les nations. Tu es grandement méprisée.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
L'orgueil de ton cœur t'a trompé, toi qui habites dans les fentes du rocher, dont la demeure est élevée, et qui dis en son cœur: Qui me fera descendre à terre?
4 Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Tu as beau monter comme l'aigle, et ton nid est placé parmi les étoiles, je t'en ferai descendre, dit Yahvé.
5 “Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
« Si des voleurs venaient chez toi, si des brigands de nuit - oh, quel désastre t'attend - ne voleraient-ils pas seulement jusqu'à ce qu'ils en aient assez? Si des vendangeurs venaient chez toi, ne laisseraient-ils pas des raisins à glaner?
6 Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
Comme Esaü sera mis à sac! Comme on cherche ses trésors cachés!
7 Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
Tous les hommes de ton alliance t'ont conduit sur ton chemin, jusqu'à la frontière. Les hommes qui étaient en paix avec toi t'ont trompé, et ont prévalu contre toi. Les amis qui mangent ton pain te tendent un piège. Il n'y a pas d'intelligence en lui. »
8 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
« Ne détruirai-je pas en ce jour-là, dit Yahvé, les sages d'Édom et l'intelligence de la montagne d'Ésaü?
9 Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
Tes vaillants hommes, Teman, seront consternés, au point que tous seront retranchés de la montagne d'Ésaü par le massacre.
10 Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
A cause de la violence faite à ton frère Jacob, la honte te couvrira, et tu seras retranché pour toujours.
11 Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
Le jour où tu t'es tenu à l'écart, le jour où des étrangers ont emporté ses biens, où des étrangers sont entrés dans ses portes et ont tiré au sort Jérusalem, toi aussi tu as été comme l'un d'eux.
12 Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
Mais ne méprise pas ton frère au jour de son malheur, et ne te réjouis pas des fils de Juda au jour de leur ruine. Ne t'enorgueillis pas au jour de la détresse.
13 Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
N'entre pas dans la porte de mon peuple au jour de son malheur. Ne méprise pas leur détresse au jour de leur calamité, et ne t'empare pas de leurs biens au jour de leur calamité.
14 Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
Ne te tiens pas aux carrefours pour couper la route à ceux qui s'échappent. Ne livre pas ceux d'entre eux qui restent au jour de la détresse.
15 “Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
Car le jour de Yahvé est proche de toutes les nations! Ce que vous avez fait, il vous sera fait. Tes actes retomberont sur ta propre tête.
16 Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
Car, comme vous avez bu sur ma montagne sainte, toutes les nations boiront sans cesse. Oui, elles boiront, elles avaleront, et elles seront comme si elles n'avaient pas été.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
Mais sur la montagne de Sion, il y aura ceux qui échapperont, et elle sera sainte. La maison de Jacob possédera ses biens.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
La maison de Jacob sera un feu, la maison de Joseph une flamme, et la maison d'Ésaü un chaume. Ils brûleront au milieu d'eux et les dévoreront. Il ne restera rien à la maison d'Ésaü. » En effet, Yahvé a parlé.
19 Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
Ceux du Sud posséderont la montagne d'Ésaü, et ceux de la plaine, les Philistins. Ils posséderont le champ d'Ephraïm et le champ de Samarie. Benjamin possédera Galaad.
20 Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
Les captifs de cette armée des enfants d'Israël, qui sont chez les Cananéens, posséderont jusqu'à Zarephath; et les captifs de Jérusalem, qui sont à Sépharad, posséderont les villes du Néguev.
21 Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.
Des sauveurs monteront sur la montagne de Sion pour juger les montagnes d'Ésaü, et le royaume sera à Yahvé.

< Obadia 1 >