< Obadia 1 >
1 Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
Obadias's Syn. Saa har den Herre, Herre sagt om Edom. Vi have hørt et Rygte fra Herren, og et Bud er sendt ud iblandt Folkene: Staar op, og lader os staa op imod det til Krig!
2 “Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
Se, jeg har gjort dig liden iblandt Folkene, du er saare foragtet.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
Dit Hjertes Hovmod har bedraget dig, du, som bor i Klippekløfter, i din høje Bolig, du, som siger i dit Hjerte: Hvo vil kaste mig ned til Jorden?
4 Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Om du end farer saa højt op som Ørnen, og om end din Rede er sat iblandt Stjernerne, vil jeg dog kaste dig ned derfra, siger Herren.
5 “Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
Hvis Tyve vare komne over dig, eller de, som anrette Ødelæggelse om Natten — ak, hvor er du dog tilintetgjort! — mon de da ikke vilde stjæle saa meget, som var dem nok? hvis Vinhøstere vare komne over dig, mon de da ikke vilde lade en Efterhøst blive tilovers?
6 Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
Hvor er dog Esau bleven gennemsøgt? hans skjulte Liggendefæ opsporet?
7 Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
Alle dine Forbundsfæller have ledsaget dig til Grænsen, de, som havde Fred med dig, have bedraget dig, de have faaet Overmagt over dig; dit Brød gøre de til en Byld under dig, — der er ingen Forstand i ham!
8 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
Mon jeg ikke paa den Dag, siger Herren, skal lade de vise forsvinde fra Edom og Forstand fra Esaus Bjerg?
9 Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
Og dine vældige, o Theman! skulle lammes af Skræk, paa det enhver maa blive udryddet fra Esaus Bjerg ved Mord.
10 Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
For Vold imod din Broder Jakob skal Skam bedække dig, og du skal udryddes evindelig.
11 Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
Paa den Dag, da du stod lige overfor, paa den Dag, da fremmede bortførte hans Gods, og Udlændinge gik ind ad hans Porte og kastede Lod over Jerusalem, har ogsaa du været som en af dem.
12 Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
Og se ej med Lyst paa din Broders Dag paa hans Ulykkesdag, og glæd dig ej over Judas Børn paa deres Undergangsdag; og tal ej hovmodigt med din Mund paa Trængselsdagen.
13 Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
Drag ej ind ad mit Folks Port paa deres Nøds Dag, se ej ogsaa du paa dets Ulykke paa dets Nøds Dag, og ræk ej efter dets Gode paa dets Nøds Dag!
14 Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
Og staa ej paa Vejskellet for at ødelægge dem, som ere undkomne derfra, og udlever ej de overblevne deraf paa Trængselsdagen!
15 “Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
Thi Herrens Dag er nær over alle Hedningerne; ligesom du har gjort, skal dig ske; Gengældelsen skal komme over dit Hoved.
16 Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
Thi ligesom I have drukket paa mit hellige Bjerg, saa skulle alle Hedningerne drikke stedse, ja, de skulle drikke og drikke ud og vorde som de, der ikke have været.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
Men paa Zions Bjerg skal der være nogle, som undkomme, og det skal være en Helligdom; og Jakobs Hus skal eje deres Ejendom.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
Og Jakobs Hus skal være en Ild og Josefs Hus en Lue, men Esaus Hus skal være til Halm, og hine skulle antænde disse og fortære dem; og der skal ingen overbleven være for Esaus Hus; thi Herren har talt det.
19 Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
Og de, som bo i Sydlandet, skulle eje Esaus Bjerg, og de, som bo i Lavlandet, skulle eje Filisterne, og de skulle eje Efraims Mark og Samarias Mark, og Benjamin skal eje Gilead.
20 Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
Og de bortførte af denne Hær af Israels Børn skulle eje det, som tilhører Kajaaniterne indtil Zarepta, og de bortførte af Jerusalem, som ere i Sefarad, de skulle eje Stæderne i Sydlandet.
21 Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.
Og Frelsere skulle drage op paa Zions Bjerg for at dømme Esaus Bjerg; og Riget skal høre Herren til.