< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
Видение Авдиино: сия глаголет Господь Бог Идумеи: слух слышах от Господа, известие во языки посла: востаните, и востанем на ню ратию.
2 “Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
Се, мала дах тя во языцех, безчестен ты еси зело.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
Презорство сердца твоего воздвиже тя живущаго в пещерах каменных: возвышаяй храмину свою, глаголяй в сердцы своем: кто мя свержет на землю?
4 Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Аще вознесешися якоже орел и аще положиши гнездо твое среде звезд, и оттуду свергу тя, глаголет Господь.
5 “Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
Аще бы татие влезли к тебе, или разбойницы нощию, камо бы повержен был еси? Еда не украли бы доволных себе? Или аще бы объемлющии виноград влезли к тебе, еда бы не оставили гроздия?
6 Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
Како обыскася Исав, и взята быша сокровенная его?
7 Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
Даже до предел испустиша тя: вси мужие завета твоего сопротивишася ти, премогоша тя мужие мирницы твои: (ядущии с тобою) положиша лесть под тобою, несть смысла в них.
8 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
В той день, глаголет Господь, погублю премудрыя от Идумеи и смысл от горы Исавовы:
9 Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
и убоятся воини твои, иже от Феман, да отимется человек от горы Исавовы.
10 Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
Посечения ради и нечестия, еже на брата твоего Иакова, покрыет тя студ, и отвержен будеши во век.
11 Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
От негоже дне сопротивился еси во дни пленяющих иноплеменников силу его, и чуждии внидоша во врата его и о Иерусалиме вергоша жребия, и ты был еси яко един от них.
12 Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
И да не презриши дне брата твоего в день чуждих, и да не порадуешися о сынех Иудиных в день погибели их, и да не велеречиши в день скорби:
13 Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
и не входи во врата людий Моих в день болезни их, и не презри и ты сонма их в день потребления их, и не совещайся на силу их в день погибели их:
14 Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
ниже настой на исходы их потребити избегающыя их, ниже заключай бежащыя их в день скорби.
15 “Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
Понеже близ день Господень на вся языки: якоже сотворил еси, сице будет ти, воздаяние твое воздастся на главу твою.
16 Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
Понеже якоже еси пил на горе Моей святей, испиют вси языцы вино, испиют и снидут, и будут яко не бывшии.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
В горе же Сиони будет спасение, и будет свята: и наследят дом Иаковль наследивших я.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
И будет дом Иаковль огнь, дом же Иосифов пламень, а дом Исавов в тростие, и возгорятся на них и поядят я, и не будет избегаяй дому Исавову, яко Господь глагола.
19 Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
И наследят иже во нагеве гору Исавову, и иже в раздолии иноплеменники: и возмут гору Ефремову и поле Самарийско, и Вениамина и Галаадитиду.
20 Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
И преселения начало сие сыном Израилевым, земля Хананейска до Сарепты: преселение же Иерусалимле до Ефрафа: и наследят грады Нагевовы.
21 Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.
И взыдут спасаемии от горы Сиони, еже отмстити гору Исавлю, и будет царство Господеви.

< Obadia 1 >