< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
Vision d’Abdias. Voici ce que dit le Seigneur Dieu à Edom: [Nous avons entendu une nouvelle venant du Seigneur; et il a envoyé un messager vers les nations: Levez-vous, et levons-nous ensemble contre lui pour le combat].
2 “Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
Voici que je t’ai placé très petit parmi les nations, tu es fort méprisable.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
L’orgueil de ton cœur t’a élevé, toi habitant dans les fentes des rochers, exaltant ton trône; toi qui dis dans ton cœur: Qui me fera descendre à terre?
4 Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Si tu t’élèves comme l’aigle, et que parmi les astres tu poses ton nid, je t’en ferai descendre, dit le Seigneur.
5 “Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
Si des voleurs, si des brigands étaient entrés chez toi durant la nuit, comment aurais-tu gardé le silence? N’auraient-ils pas volé ce qui leur suffisait? Si des vendangeurs étaient entrés chez toi, est-ce qu’ils ne t’auraient pas laissé au moins une grappe de raisin?
6 Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
Comment les ennemis ont-ils fouillé Esaü, fureté dans ce qu’il avait de caché?
7 Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
Ils t’ont éconduit jusqu’à la frontière; tous tes alliés se sont joués de toi; les hommes qui vivaient en paix avec toi ont prévalu contre toi; ceux qui mangent ton pain dresseront des embûches sous tes pas; il n’y a pas de prudence en lui.
8 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
N’est-ce pas en ce jour-là, dit le Seigneur, que je perdrai les sages de l’Idumée et bannirai la prudence de la montagne d’Esaü?
9 Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
Et ils craindront, tes braves du midi, que l’homme de la montagne d’Esaü ne périsse.
10 Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
À cause de tes meurtres et à cause de ton iniquité contre Jacob ton frère, la confusion te couvrira, et tu périras pour jamais.
11 Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
Au jour que tu t’élevais contre lui, quand des ennemis se rendaient maîtres de son armée, et que des étrangers entraient dans ses portes, et que sur Jérusalem ils jetaient le sort, toi aussi tu étais comme l’un d’entre eux.
12 Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
Et tu ne mépriseras pas ton frère en son jour malheureux, au jour de son exil, et tu ne te réjouiras pas sur les fils de Juda au jour de leur ruine; et tu ne parleras pas orgueilleusement au jour de l’angoisse.
13 Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
Et tu n’entreras pas dans la porte de mon peuple au jour de leur ruine; et tu ne les mépriseras pas, toi non plus, au milieu de ses maux, au jour de sa désolation; et tu ne seras pas envoyé contre son armée au jour de sa désolation.
14 Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
Et tu ne te tiendras pas dans les carrefours, afin de tuer ceux qui fuiront, et tu n’enfermeras pas les restes de ses habitants au jour de la tribulation.
15 “Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
Parce que le jour du Seigneur est près d’éclater sur toutes les nations; comme tu as fait, il te sera fait; ce que tu leur as fait, il le fera retomber sur ta tête.
16 Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
Car comme vous avez bu sur ma montagne sainte, toutes les nations boiront sans discontinuer; et elles boiront, elles avaleront, et elles seront comme si elles n’étaient point.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
Mais sur la montagne de Sion sera le salut et elle sera sainte: la maison de Jacob possédera ceux qui l’avaient possédée.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
Et la maison de Jacob sera un feu, et la maison de Joseph une flamme, et la maison d’Esaü une paille; et ils l’embraseront, et ils la dévoreront, et il n’y aura pas de restes de la maison d’Esaü, parce que le Seigneur a parlé.
19 Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
Et ceux qui sont au midi hériteront de la montagne d’Esaü; et ceux qui sont dans les plaines assujettiront les Philistins; et ils posséderont la contrée d’Ephraïm et la contrée de Samarie, et Benjamin possédera Galaad.
20 Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
Et les exilés de cette armée des enfants d’Israël posséderont tous les lieux des Chananéens jusqu’à Sarepta; et les exilés de Jérusalem, qui sont sur le Bosphore, posséderont les cités du midi.
21 Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.
Et les libérateurs monteront sur la montagne de Sion pour juger la montagne d’Esaü; et le règne sera au Seigneur.

< Obadia 1 >