< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
Visioun of Abdias. The Lord God seith these thingis to Edom. We herden an heryng of the Lord, and he sente a messanger to hethene men. Rise ye, and togidere rise we ayens hym in to batel.
2 “Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
Lo! Y yaf thee litil in hethene men, thou art ful myche `worthi to be dispisid.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
The pride of thin herte enhaunside thee, dwellynge in crasyngis of stoonys, areisynge thi seete. Whiche seist in thin herte, Who schal drawe me doun in to erthe?
4 Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Thouy thou schalt be reisid as an egle, and thouy thou schalt putte thi nest among sterris, fro thennus Y schal drawe thee doun, seith the Lord.
5 “Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
If niyt theuys hadden entrid to thee, if outlawis bi niyt, hou schuldist thou haue be stille? whether thei schulden not haue stole thingis ynow to hem? If gadereris of grapis hadden entrid to thee, whether thei schulden haue left nameli clustris to thee?
6 Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
Hou souyten thei Esau, serchiden the hid thingis of him?
7 Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
Til to the termes thei senten out thee; and alle men of thi couenaunt of pees scorneden thee, men of thi pees wexiden stronge ayens thee; thei that schulen ete with thee, schulen put aspies, ether tresouns, vndur thee; ther is no prudence in hym.
8 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
Whether not in that dai, seith the Lord, Y schal lese the wise men of Idumee, and prudence of the mount of Esau?
9 Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
And thi stronge men schulen drede of myddai, that a man of the hil of Esau perische.
10 Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
For sleyng and for wickidnesse ayens thi brother Jacob, confusioun schal hile thee, and thou schalt perische with outen ende.
11 Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
In the dai whanne thou stodist ayens hym, whanne aliens token the oost of hym, and straungeris entriden the yatis of hym, and senten lot on Jerusalem, thou were also as oon of hem.
12 Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
And thou schalt not dispise in the dai of thi brother, in the dai of his pilgrimage, and thou schalt not be glad on the sones of Juda, in the dai of perdicioun of hem; and thou schalt not magnefie thi mouth in the dai of angwisch,
13 Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
nether schalt entre in to the yate of my puple, in the dai of fallyng of hem; and thou schalt not dispise in the yuels of hym, in the dai of his distriyng; and thou schalt not be sent out ayens his oost, in the day of his distriyng;
14 Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
nether thou schalt stonde in the goynges out, that thou sle hem that fledden; and thou schalt not close togidere the residues, ether left men, of hym, in the day of tribulacioun,
15 “Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
for the dai of the Lord is niy on alle `hethene men. As thou hast doon, it schal be doon to thee; he schal conuerte thi yeldyng in to thin heed.
16 Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
For as ye drunken on myn hooli hil, alle hethene men schulen drynke bisili, and thei schulen drynke, and schulen soupe vp; and thei schulen be as if thei ben not.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
And saluacioun schal be in the hil of Sion, and it schal be hooli; and the hous of Jacob schal welde hem whiche weldiden hem.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
And the hous of Jacob schal be fier, and the hous of Joseph schal be flawme, and the hous of Esau schal be stobil; and `thei schulen be kyndlid in hem, and thei schulen deuoure hem; and relifs schulen not be of the hous of Esau, for the Lord spak.
19 Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
And these that ben at the south, schulen enherite the hil of Esau; and thei that ben in the lowe feeldis, schulen enherite Filistiym; and thei schulen welde the cuntrei of Effraym, and cuntrei of Samarie; and Beniamyn schal welde Galaad.
20 Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
And ouerpassyng of this oost of sones of Israel schal welde alle places of Cananeis, til to Sarepta; and the transmygracioun of Jerusalem, that is in Bosphoro, schal welde citees of the south.
21 Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.
And sauyours schulen stie in to the hil of Sion, for to deme the hil of Esau, and a rewme schal be to the Lord.

< Obadia 1 >