< Hesabu 1 >
1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
Och Herren talade med Mose, i Sinai öken, uti vittnesbördsens tabernakel, på första dagen, i den andra månadenom, i de andra årena, sedan de voro gångne utur Egypti land, och sade:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
Tager en summo af hela Israels barnas menighet, efter deras slägter, och deras fäders hus och namn, allt det som mankön är, ifrå hufvud till hufvud;
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
Ifrå tjugu år och derutöfver, allt det som doger till att draga i här i Israel. Och I skolen tälja dem efter deras härar, du och Aaron;
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Och skolen taga till eder af hvarjo slägtene en höfvitsman öfver hans faders hus.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
Desse äro namnen af de höfvitsmän, som med eder stå skola. Af Ruben: Elizur, Sedeurs son.
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
Af Simeon: Selumiel, ZuriSadai son.
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
Af Juda: Nahesson, Amminadabs son.
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
Af Isaschar: Nethaneel, Zuars son.
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
Af Sebulon: Eliab, Helons son.
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
Af Josephs barn: Af Ephraim, Elisama, Ammihuds son: Af Manasse, Gamliel, Pedahzurs son.
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
Af BenJamin: Abidan, Gideoni son.
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
Af Dan: Ahieser, Ammi Sadai son.
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
Af Asser: Pagiel, Ochrans son.
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
Af Gad: Eliasaph, Deguels son.
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
Af Naphthali: Ahira, Enans son.
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
Desse äro de namnkunnigaste i menighetene, höfvitsmän i deras fäders slägter, som voro hufvud och Förstar i Israel.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
Och Mose och Aaron togo dem till sig, såsom de vid namn uppräknade voro;
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
Och församlade desslikes hela menighetena på första dagen i den andra månadenom, och räknade dem efter deras börd, efter deras slägter och fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, ifrå hufvud till hufvud;
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Såsom Herren hade budit Mose; och talde dem uti Sinai öken.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Rubens barn, som var den förste Israels son, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå hufvud till hufvud, allt det mankön var, ifrå tjugu år och derutöfver, och de som dogde till att draga i här,
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
De vordo räknade intill Rubens slägte, sex och fyratio tusend, och femhundrad.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Simeons barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå hufvud till hufvud, allt det som mankön var, ifrå tjugu år och derutöfver, och i här draga dogde,
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
Vordo talde intill Simeons slägte, nio och femtio tusend, och trehundrad.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Gads barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det som i här draga dogde,
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
Vordo talde intill Gads slägte, fem och fyratio tusend, sexhundrad och femtio.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Juda barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde,
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
Vordo talde intill Juda slägte, fyra och sjutio tusend, och sexhundrad.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Isaschars barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde,
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
Vordo talde intill Isaschars slägte, fyra och femtio tusend, och fyrahundrad.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Sebulons barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde,
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
Vordo talde intill Sebulons slägte, sju och femtio tusend, och fyrahundrad.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Josephs barn, af Ephraim, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde,
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
Vordo talde intill Ephraims slägte, fyratiotusend, och femhundrad.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Manasse barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde,
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
Vordo talde intill Manasse slägte, tu och tretio tusend, och tuhundrad.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
BenJamins barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde,
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
Vordo talde intill BenJamins slägte, fem och tretio tusend, och fyrahundrad.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dans barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde,
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
Vordo talde intill Dans slägte, tu och sextio tusend, och sjuhundrad.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Assers barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde.
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
Vordo talde intill Assers slägte, ett och fyratio tusend, och femhundrad.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Naphthali barn, efter deras börd, slägter, deras fäders hus och namn, ifrå tjugu år och derutöfver, allt det i här draga dogde,
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
Vordo talde intill Naphthali slägte, tre och femtio tusend, och fyrahundrad.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
Desse äro de som Mose och Aaron, samt med de tolf Israels Förstar, talde, af hvilkom ju en var öfver hvart af deras fäders hus.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Och summan af Israels barn, efter deras fäders hus, ifrå tjugu år och derutöfver, det i här draga dogde i Israel,
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
Var sex resor hundradetusend, och tretusen, femhundrade och femtio.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Men de Leviter, efter deras fäders slägter, vordo intet räknade ibland med.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
Och Herren talade med Mose, och sade:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
Levi slägt skall du intet räkna, eller taga någon summo af dem, ibland Israels barn.
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
Men du skall skicka dem till vittnesbördsens tabernakel, och till all dess tyg, och allt det dertill hörer; och de skola bära tabernaklet, och all dess tyg, och skola det sköta, och lägra sig omkring tabernaklet.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
Och när man resa skall, då skola de Leviter taga tabernaklet neder; och när hären skall lägra sig, skola de slå tabernaklet upp. Om någor främmande nalkas dertill, han skall dö.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
Israels barn skola lägra sig hvar i sitt lägre, och vid sins härs baner.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Men Leviterna skola lägra sig omkring vittnesbördsens tabernakel, på det icke skall komma en vrede öfver menighetena af Israels barn. Derföre skola de Leviter vakt hålla vid vittnesbördsens tabernakel.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Och Israels barn gjorde allt det Herren Mose budit hade.