< Hesabu 1 >

1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
Fallou mais o Senhor a Moysés no deserto de Sinai, na tenda da congregação, no primeiro dia do mez segundo no segundo anno da sua saida da terra do Egypto, dizendo:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
Tomae a somma de toda a congregação dos filhos d'Israel, segundo as suas gerações, segundo a casa de seus paes, no numero dos nomes de todo o macho, cabeça por cabeça;
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
Da edade de vinte annos e para cima, todos os que saem á guerra em Israel: a estes contareis segundo os seus exercitos, tu e Aarão.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Estará comvosco de cada tribu um homem que seja cabeça da casa de seus paes,
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
Estes pois são os nomes dos homens que estarão comvosco: De Ruben, Elizur, filho de Sedeur;
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
De Simeão, Selumiel, filho de Surisaddai;
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
De Judah, Naasson, filho de Amminadab;
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
D'Issacar, Nathanael, filho de Suhar;
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
De Zebulon, Eliab, filho de Helon;
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
Dos filhos de José: d'Ephraim; Elisama, filho d'Ammihud; de Manasseh, Gamaliel, filho de Pedazur;
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
De Benjamin, Abidan, filho de Gideoni;
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
De Dan, Ahieser, filho de Ammisaddai;
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
De Aser, Pagiel, filho d'Ochran;
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
De Gad, Eliasaph, filho de Dehuel;
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
De Naphtali, Ahira, filho d'Enan.
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
Estes foram os chamados da congregação, os principes das tribus de seus paes, os Cabeças dos milhares d'Israel.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
Então tomaram Moysés e Aarão a estes homens, que foram declarados pelos seus nomes.
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
E ajuntaram toda a congregação no primeiro dia do mez segundo, e declararam a sua descendencia segundo as suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, cabeça por cabeça;
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Como o Senhor ordenara a Moysés, assim os contou no deserto de Sinai.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Foram pois os filhos de Ruben, o primogenito d'Israel; as suas gerações pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes, cabeça por cabeça, todo o macho de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra;
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
Foram contados d'elles, da tribu de Ruben, quarenta e seis mil e quinhentos.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de Simeão, as suas gerações pelas suas familias, segundo a casa dos seus paes; os seus contados, pelo numero dos nomes, cabeça por cabeça, todo o macho de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
Foram contados d'elles, da tribu de Simeão, cincoenta e nove mil e trezentos.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de Gad, as suas gerações pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
Foram contados d'elles, da tribu de Gad, quarenta e cinco mil e seiscentos e cincoenta.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de Judah, as suas gerações pelas suas familias, segundo a casa de seus paes; pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
Foram contados d'elles, da tribu de Judah, setenta e quatro mil e seiscentos.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos d'Issacar, as suas gerações pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
Foram contados d'elles, da tribu d'Issacar, cincoenta e quatro mil e quatrocentos.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de Zebulon, as suas gerações, pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
Foram contados d'elles, da tribu de Zebulon, cincoenta e sete mil e quatrocentos.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de José, dos filhos d'Ephraim, as suas gerações, pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
Foram contados d'elles, da tribu d'Ephraim, quarenta mil e quinhentos.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de Manasseh, as suas gerações, pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
Foram contados d'elles, da tribu de Manasseh, trinta e dois mil e duzentos.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de Benjamin, as suas gerações, pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
Foram contados d'elles, da tribu de Benjamin, trinta e cinco mil e quatrocentos.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de Dan, as suas gerações, pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
Foram contados d'elles, da tribu de Dan, sessenta e dois mil e setecentos.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos d'Aser, as suas gerações, pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
Foram contados d'elles, da tribu d'Aser, quarenta e um mil e quinhentos.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dos filhos de Naphtali, as suas gerações, pelas suas familias, segundo a casa de seus paes, pelo numero dos nomes dos de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra,
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
Foram contados d'elles, da tribu de Naphtali, cincoenta e tres mil e quatrocentos.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
Estes foram os contados, que contou Moysés e Aarão, e os principes d'Israel, doze homens, cada um era pela casa de seus paes.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Assim foram todos os contados dos filhos d'Israel, segundo a casa de seus paes, de vinte annos e para cima, todos os que podiam sair á guerra em Israel;
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
Todos os contados pois foram seiscentos e tres mil e quinhentos e cincoenta.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Mas os levitas, segundo a tribu de seus paes, não foram contados entre elles,
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
Porquanto o Senhor tinha fallado a Moysés, dizendo:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
Porém não contarás a tribu de Levi, nem tomarás a somma d'elles entre os filhos d'Israel:
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
Mas tu põe os levitas sobre o tabernaculo do testemunho, e sobre todos os seus vasos, e sobre tudo o que pertence a elle: elles levarão o tabernaculo e todos os seus vasos; e elles o administrarão, e assentarão o seu arraial ao redor do tabernaculo.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
E, quando o tabernaculo partir, os levitas o desarmarão; e, quando o tabernaculo assentar no arraial, os levitas o armarão; e o estranho que se chegar morrerá.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
E os filhos d'Israel assentarão as suas tendas, cada um no seu esquadrão, e cada um junto á sua bandeira, segundo os seus exercitos.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Mas os levitas assentarão as suas tendas ao redor do tabernaculo do testemunho, para que não haja indignação sobre a congregação dos filhos d'Israel, pelo que os levitas terão o cuidado da guarda do tabernaculo do testemunho.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Assim fizeram os filhos d'Israel: conforme a tudo o que o Senhor ordenara a Moysés, assim o fizeram.

< Hesabu 1 >