< Hesabu 1 >

1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
Locutusque est Dominus ad Moysen in deserto Sinai in tabernaculo foederis, prima die mensis secundi, anno altero egressionis eorum ex Aegypto, dicens:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
Tollite summam universae congregationis filiorum Israel per cognationes et domos suas, et nomina singulorum, quidquid sexus est masculini
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
a vigesimo anno et supra, omnium virorum fortium ex Israel, et numerabitis eos per turmas suas, tu et Aaron.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Eruntque vobiscum principes tribuum ac domorum in cognationibus suis,
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
quorum ista sunt nomina: De Ruben, Elisur filius Sedeur.
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
de Simeon, Salamiel filius Surisaddai.
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
de Iuda, Nahasson, filius Aminadab.
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
de Issachar, Nathanael filius Suar.
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
de Zabulon, Eliab filius Helon.
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
Filiorum autem Ioseph, de Ephraim, Elisama filius Ammiud. de Manasse, Gamaliel filius Phadasseur.
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
De Beniamin, Abidan filius Gedeonis.
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
de Dan, Ahiezer filius Ammisaddai.
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
de Aser, Phegiel filius Ochran.
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
de Gad, Eliasaph filius Duel.
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
de Nephthali, Ahira filius Enan.
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
Hi nobilissimi principes multitudinis per tribus et cognationes suas, et capita exercitus Israel:
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
quos tulerunt Moyses et Aaron cum omni vulgi multitudine:
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
et congregaverunt primo die mensis secundi, recensentes eos per cognationes, et domos, ac familias, et capita, et nomina singulorum a vigesimo anno et supra,
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
sicut praeceperat Dominus Moysi. Numeratique sunt in deserto Sinai.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De Ruben primogenito Israelis per generationes et familias ac domos suas, et nomina capitum singulorum, omne quod sexus est masculini a vigesimo anno et supra, procedentium ad bellum,
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
quadraginta sex millia quingenti.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Simeon per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina et capita singulorum, omne quod sexus est masculini a vigesimo anno et supra, procedentium ad bellum,
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
quinquaginta novem millia trecenti.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Gad per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a viginti annis et supra, omnes qui ad bella procederent,
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
quadragintaquinque millia sexcenti quinquaginta.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Iuda per generationes et familias ac domos cognationum suarum, per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
recensiti sunt septuaginta quattuor millia sexcenti.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Issachar, per generationes et familias ac domos cognationum suarum, per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui ad bella procederent,
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
recensiti sunt quinquaginta quattuor millia quadringenti.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Zabulon per generationes et familias, ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
quinquaginta septem millia quadringenti.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Ioseph, filiorum Ephraim per generationes, et familias, ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
quadraginta millia quingenti.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Porro filiorum Manasse per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a viginti annis et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
triginta duo millia ducenti.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Beniamin per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt nominibus singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
triginta quinque millia quadringenti.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Dan per generationes, et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt nominibus singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
sexaginta duo millia septingenti.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Aser per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
quadraginta millia et mille quingenti.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
De filiis Nephthali per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt nominibus singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
quinquaginta tria millia quadringenti.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
Hi sunt, quos numeraverunt Moyses et Aaron, et duodecim principes Israel, singulos per domos cognationum suarum.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Fueruntque omnis numerus filiorum Israel per domos et familias suas a vigesimo anno et supra, qui poterant ad bella procedere,
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
sexcenta tria millia virorum quingenti quinquaginta.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Levitae autem in tribu familiarum suarum non sunt numerati cum eis.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
Locutusque est Dominus ad Moysen, dicens:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
Tribum Levi noli numerare, neque pones summam eorum cum filiis Israel:
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
sed constitue eos super tabernaculum testimonii et cuncta vasa eius, et quidquid ad ceremonias pertinet. Ipsi portabunt tabernaculum et omnia utensilia eius: et erunt in ministerio, ac per gyrum tabernaculi metabuntur.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
Cum proficiscendum fuerit, deponent Levitae tabernaculum: cum castrametanda, erigent. quisquis externorum accesserit, occidetur.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
Metabuntur autem castra filii Israel unusquisque per turmas et cuneos atque exercitum suum.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Porro Levitae per gyrum tabernaculi figent tentoria, ne fiat indignatio super multitudinem filiorum Israel, et excubabunt in custodiis tabernaculi testimonii.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Fecerunt ergo filii Israel iuxta omnia quae praeceperat Dominus Moysi.

< Hesabu 1 >