< Hesabu 1 >

1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
Yahweh parla à Moïse au désert de Sinaï, dans la tente de réunion, le premier jour du second mois, la deuxième année après leur sortie du pays d’Égypte, en disant:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
« Faites le compte de toute l’assemblée des enfants d’Israël, selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant par tête le nom de tous les mâles
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes aptes à porter les armes en Israël; vous en ferez le dénombrement selon leurs troupes, toi et Aaron.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Il y aura avec vous un homme de chaque tribu, chef de sa maison patriarcale.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
Voici les noms de ceux qui se tiendront avec vous: Pour Ruben: Elisur, fils de Sédéur;
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
pour Siméon: Salamiel, fils de Surisaddaï;
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
pour Juda: Nahasson, fils d’Aminadab;
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
pour Issachar: Nathanaël, fils de Suar;
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
pour Zabulon: Eliab, fils de Hélon;
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
pour les fils de Joseph, pour Ephraïm: Elisama, fils d’Ammiud; pour Manassé: Gamaliel, fils de Phadassur;
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
pour Benjamin: Abidan, fils de Gédéon;
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
pour Dan: Ahiéser, fils d’Ammisaddaï;
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
pour Aser: Phégiel, fils d’Ochran;
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
pour Gad: Eliasaph, fils de Duel;
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
pour Nephtali: Ahira, fils d’Enan. »
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
Tels sont ceux qui furent appelés de l’assemblée; ils étaient princes des tribus de leurs pères, chefs des milliers d’Israël.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
Moïse et Aaron, ayant pris ces hommes qui avaient été désignés par leurs noms,
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
convoquèrent toute l’assemblée pour le premier jour du deuxième mois. Et ils furent enregistrés selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant par tête les noms, depuis l’âge de vingt et au-dessus.
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Comme Yahweh l’avait ordonné à Moïse, celui-ci en fit le dénombrement dans le désert de Sinaï.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Ruben, premier-né d’Israël, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms par tête, tous les mâles depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter des armes:
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
les recensés de la tribu de Ruben furent quarante-six mille cinq cents.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Siméon, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, leurs recensés en comptant les noms par tête, tous les mâles depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
les recensés de la tribu de Siméon furent cinquante-neuf mille trois cents.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Gad, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
les recensés de la tribu de Gad furent quarante-cinq mille six cent cinquante.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Juda, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
les recensés de la tribu de Juda furent soixante-quatorze mille six cents.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils d’Issachar, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
les recensés de la tribu d’Issachar furent cinquante-quatre mille quatre cents.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Zabulon, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
les recensés de la tribu de Zabulon furent cinquante-sept mille quatre cents.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Joseph, — fils d’Ephraïm, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
les recensés de la tribu d’Ephraïm furent quarante mille cinq cents.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
— Fils de Manassé, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
les recensés de la tribu de Manassé furent trente-deux mille deux cents.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Benjamin, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
les recensés de la tribu de Benjamin furent trente-cinq mille quatre cents.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Dan, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
les recensés de la tribu de Dan furent soixante-deux mille sept cents.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils d’Aser, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
les recensés de la tribu d’Aser furent quarante et un mille cinq cents.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Fils de Nephtali, leurs descendants selon leurs familles, selon leurs maisons patriarcales, en comptant les noms depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes en état de porter les armes:
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
les recensés de la tribu de Nephtali furent cinquante-trois mille quatre cents.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
Tels sont ceux qui furent recensés, que recensèrent Moïse et Aaron, avec les princes d’Israël, au nombre de douze: un homme pour chacune de leurs maisons patriarcales.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Tous les enfants d’Israël dont on fit le recensement, selon leurs maisons patriarcales, depuis l’âge de vingt ans et au-dessus, tous les hommes d’Israël en état de porter les armes,
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
tous les recensés furent six cent trois mille cinq cent cinquante.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Les Lévites, selon leur tribu patriarcale, ne furent pas recensés avec eux.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
Yahweh parla à Moïse, en disant:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
« Tu ne feras pas le recensement de la tribu de Lévi, et tu n’en réuniras pas le compte avec celui des enfants d’Israël.
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
Remets à leur soin la demeure du témoignage, tous ses ustensiles et tout ce qui lui appartient. Ils porteront la Demeure et tous ses ustensiles, ils en feront le service, et ils camperont autour de la Demeure.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
Quand la Demeure partira, les Lévites la démonteront; quand la Demeure campera, les Lévites la dresseront; et l’étranger qui s’en approchera sera puni de mort.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
Les enfants d’Israël camperont chacun dans son camp, chacun près de sa bannière, selon leurs troupes.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Mais les Lévites camperont autour de la Demeure du témoignage, afin que ma colère n’éclate point sur l’assemblée des enfants d’Israël; et les Lévites auront la garde de la Demeure du témoignage. »
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Les enfants d’Israël agirent selon tout ce que Yahweh avait ordonné à Moïse; ils firent ainsi.

< Hesabu 1 >