< Hesabu 1 >

1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
And Jehovah spoke to Moses in the wilderness of Sinai in the tent of meeting, on the first of the second month, in the second year after their departure from the land of Egypt, saying,
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
Take the sum of the whole assembly of the children of Israel, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, every male, according to their polls;
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
from twenty years and upward, all that go forth to military service in Israel: ye shall number them according to their hosts, thou and Aaron.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
And with you there shall be a man for every tribe, a man who is the head of his father's house.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
And these are the names of the men that shall stand with you: for Reuben, Elizur the son of Shedeur;
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
for Simeon, Shelumiel the son of Zurishaddai;
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
for Judah, Nahshon the son of Amminadab;
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
for Issachar, Nethaneel the son of Zuar;
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
for Zebulun, Eliab the son of Helon;
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
for the children of Joseph: for Ephraim, Elishama the son of Ammihud; for Manasseh, Gamaliel the son of Pedahzur;
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
for Benjamin, Abidan the son of Gideoni;
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
for Dan, Ahiezer the son of Ammishaddai;
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
for Asher, Pagiel the son of Ocran;
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
for Gad, Eliasaph the son of Deuel;
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
for Naphtali, Ahira the son of Enan.
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
These were those summoned of the assembly, princes of the tribes of their fathers, the heads of the thousands of Israel.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
And Moses and Aaron took these men who are expressed by their names,
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
and gathered the whole assembly together on the first of the second month. And they declared their pedigrees after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, according to their polls.
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
As Jehovah had commanded Moses, so he numbered them in the wilderness of Sinai.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
And the sons of Reuben, Israel's eldest son, their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, according to their polls, every male from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
those that were numbered of them, of the tribe of Reuben, were forty-six thousand five hundred.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Simeon: their generations, after their families, according to their fathers' houses, those that were numbered of them, by the number of the names, according to their polls, every male from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
those that were numbered of them, of the tribe of Simeon, were fifty-nine thousand three hundred.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Gad: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
those that were numbered of them, of the tribe of Gad, were forty-five thousand six hundred and fifty.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Judah: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
those that were numbered of them, of the tribe of Judah, were seventy-four thousand six hundred.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Issachar: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
those that were numbered of them, of the tribe of Issachar, were fifty-four thousand four hundred.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Zebulun: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
those that were numbered of them, of the tribe of Zebulun, were fifty-seven thousand four hundred.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Joseph: of the children of Ephraim: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
those that were numbered of them, of the tribe of Ephraim, were forty thousand five hundred.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the children of Manasseh: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
those that were numbered of them, of the tribe of Manasseh, were thirty-two thousand two hundred.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Benjamin: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
those that were numbered of them, of the tribe of Benjamin, were thirty-five thousand four hundred.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Dan: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
those that were numbered of them, of the tribe of Dan, were sixty-two thousand seven hundred.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Asher: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
those that were numbered of them, of the tribe of Asher, were forty-one thousand five hundred.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of the sons of Naphtali: their generations, after their families, according to their fathers' houses, by the number of the names, from twenty years old and upward, all that went forth to military service:
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
those that were numbered of them, of the tribe of Naphtali, were fifty-three thousand four hundred.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
These are those that were numbered, whom Moses and Aaron numbered, and the princes of Israel, the twelve men: each one was for the house of his fathers.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
And all those that were numbered of the children of Israel, according to their fathers' houses, from twenty years old and upward, all that went forth to military service in Israel,
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
all they that were numbered were six hundred and three thousand five hundred and fifty.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
But the Levites after the tribe of their fathers were not numbered among them.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
For Jehovah had spoken to Moses, saying,
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
Only thou shalt not number the tribe of Levi, neither take the sum of them among the children of Israel.
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
But thou, appoint the Levites over the tabernacle of testimony, and over all the vessels thereof, and over all things that belong to it: they shall bear the tabernacle, and all its vessels; and they shall serve it, and round about the tabernacle shall they encamp;
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
and when the tabernacle setteth forward, the Levites shall take it down; and when the tabernacle encampeth, the Levites shall set it up; and the stranger that cometh near shall be put to death.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
And the children of Israel shall encamp every man in his camp, and every man by his own standard, according to their hosts;
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
but the Levites shall encamp round about the tabernacle of testimony, that there come not wrath upon the assembly of the children of Israel; and the Levites shall keep the charge of the tabernacle of testimony.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
And the children of Israel did so; according to all that Jehovah had commanded Moses, so did they.

< Hesabu 1 >