< Hesabu 1 >
1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
Og Herren talede til Mose i Sinai Ørk i Forsamlingens Paulun paa den første Dag i den anden Maaned i det andet Aar, efter at de vare udgangne af Ægyptens Land, og sagde:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
Tager Hovedsum paa hele Israels Børns Menighed, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, ved Navnes Tal, alt Mandkøn Hoved for Hoved af dem,
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
fra tyve Aar gamle og derover, hver som kan uddrage i Krig udi Israel; I skulle tælle dem efter deres Hær, du og Aron.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
Og med eder skal være en Mand for hver Stamme, en Mand, som er Øverste for sit Fædrenehus.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
Og disse ere Navnene paa Mændene, som skulle staa eder bi: For Ruben: Elizur, Sedeurs Søn;
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
for Simeon: Selumiel, Zurisaddai Søn;
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
for Juda: Nahesson, Amminadabs Søn;
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
for Isaskar: Nethaneel, Zuars Søn;
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
for Sebulon: Eliab, Helons Søn;
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
for Josefs Børn, for Efraim: Elisama, Amihuds Søn; for Manasse: Gamliel, Pedazurs Søn;
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
for Benjamin: Abidan, Gideoni Søn;
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
for Dan: Ahieser, Ammisaddai Søn;
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
for Aser: Pagiel, Okrans Søn;
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
for Gad: Eliasaf, Deuels Søn;
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
for Nafthali: Ahira, Enans Søn.
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
Disse vare de kaldte af Menigheden, Fyrster for deres Fædres Stammer; de vare Øverster for Israels Tusinder.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
Og Mose og Aron toge disse Mænd, som ere udtrykkelig nævnede ved Navne.
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
Og de lode hele Menigheden samle sig paa den første Dag i den anden Maaned, og de opgave deres Herkomst, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, Hoved for Hoved.
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Som Herren havde befalet Mose, saa talte han dem i Sinai Ørk.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Og Rubens, Israels førstefødtes, Børns Afkom efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, Hoved for Hoved, alt Mandkøn fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
De talte af dem til Rubens Stamme vare seks og fyrretyve Tusinde og fem Hundrede.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Simeons Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus; de talte af dem efter Navnes Tal, Hoved for Hoved, alt Mandkøn fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
De talte af dem til Simeons Stamme vare ni og halvtredsindstyve Tusinde og tre Hundrede.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Gads Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
De talte af dem til Gads Stamme vare fem og fyrretyve Tusinde og seks Hundrede og halvtredsindstyve.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Judas Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
De talte af dem til Judas Stamme vare fire og halvfjerdsindstyve Tusinde og seks Hundrede.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Isaskars Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
De talte af dem til Isaskars Stamme vare fire og halvtredsindstyve Tusinde og fire Hundrede.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Sebulons Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
De talte af dem til Sebulons Stamme vare syv og halvtredsindstyve Tusinde og fire Hundrede.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Josefs Børn, nemlig Efraims Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
De talte af dem til Efraims Stamme vare fyrretyve Tusinde og fem Hundrede.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Manasse Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
De talte af dem til Manasse Stamme vare to og tredive Tusinde og to Hundrede.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Benjamins Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
De talte af dem til Benjamins Stamme vare fem og tredive Tusinde og fire Hundrede.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Dans Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
De talte af dem til Dans Stamme vare to og tresindstyve Tusinde og syv Hundrede.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Asers Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
De talte af dem til Asers Stamme vare eet og fyrretyve Tusinde og fem Hundrede.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Nafthali Børns Afkom, efter deres Slægter, efter deres Fædrenehus, efter Navnes Tal, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid:
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
De talte af dem til Nafthali Stamme vare tre og halvtredsindstyve Tusinde og fire Hundrede.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
Disse ere de talte, som Mose og Aron talte, og hver af de tolv Israels Fyrster; hver Mand var for sit Fædrenehus.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
Og alle de, som bleve talte af Israels Børn, efter deres Fædrenehus, fra tyve Aar gamle og derover, hver som kunde uddrage i Strid i Israel,
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
ja, alle de talte vare seks Hundrede Tusinde og tre Tusinde og fem Hundrede og halvtredsindstyve.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
Men Leviterne efter deres Fædres Stamme, de bleve ikke talte iblandt dem.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
Thi Herren talede til Mose og sagde:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
Dog skal du ikke tælle Levi Stamme og ej tage Hovedsum paa dem, midt iblandt Israels Børn;
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
men du skal beskikke Leviterne over Vidnesbyrdets Tabernakel og over alt Redskabet dertil og over alt det, som dertil hører, de skulle bære Tabernaklet og alt Redskabet dertil, og de skulle tjene ved det; og de skulle lejre sig trindt omkring Tabernaklet.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
Og naar Tabernaklet skal rejse, skulle Leviterne tage det ned; men naar Tabernaklet skal lejre sig, skulle Leviterne rejse det op; og kommer nogen fremmed nær derved, skal han dødes.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
Og Israels Børn skulle lejre sig, hver i sin Lejr og hver hos sit Banner efter deres Hære.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
Men Leviterne skulle lejre sig omkring Vidnesbyrdets Tabernakel, at ikke en Vrede skal være over Israels Børns Menighed; derfor skulle Leviterne tage Vare paa, hvad der er at varetage ved Vidnesbyrdets Tabernakel.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Og Israels Børn gjorde det; efter alt det, som Herren havde befalet Mose, saa gjorde de.