< Hesabu 8 >
2 “Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
“Harun'a de ki, yedi kandili kandilliğin önünü aydınlatacak biçimde yerleştirsin.”
3 Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Harun söyleneni yaptı. RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi, kandilleri kandilliğin önüne yerleştirdi.
4 Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
Kandillik, ayağından çiçek motiflerine dek dövme altından, RAB'bin Musa'ya gösterdiği örneğe göre yapıldı.
6 “Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
“Levililer'i İsrailliler'in arasından ayırıp dinsel açıdan arındır.
7 Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
Onları arındırmak için şöyle yapacaksın: Günahtan arındırma suyunu üzerlerine serp; bedenlerindeki bütün kılları tıraş etmelerini, giysilerini yıkamalarını sağla. Böylece arınmış olurlar.
8 Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Sonra bir boğa ile tahıl sunusu için zeytinyağıyla yoğrulmuş ince un alsınlar; günah sunusu için sen de başka bir boğa alacaksın.
9 Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
Levililer'i Buluşma Çadırı'nın önüne getir, bütün İsrail topluluğunu da topla.
10 Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
Levililer'i RAB'bin huzuruna getireceksin, İsrailliler ellerini üzerlerine koyacaklar.
11 Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
Harun, RAB'bin hizmetini yapabilmeleri için, İsrailliler'in arasından adak olarak Levililer'i RAB'be adayacak.
12 “Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
“Levililer ellerini boğaların başına koyacaklar; günahlarını bağışlatmak için boğalardan birini günah sunusu, öbürünü yakmalık sunu olarak RAB'be sunacaksın.
13 Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Levililer Harun'la oğullarının önünde duracaklar. Onları adak olarak RAB'be adayacaksın.
14 Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
Levililer'i öbür İsrailliler'in arasından bu şekilde ayıracaksın. Levililer benim olacak.
15 “Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
“Sen onları arındırıp adak olarak adadıktan sonra, Levililer Buluşma Çadırı'ndaki hizmeti yerine getirmeye başlayacaklar.
16 Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
Çünkü İsrailliler arasından Levililer tümüyle bana verilmiştir. İlk doğanların, İsrailli kadınların doğurdukları ilk erkek çocukların yerine onları kendime ayırdım.
17 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
İsrailliler arasında ilk doğan insan ya da hayvan benimdir. Mısır'da ilk doğanları yok ettiğim gün, onları kendime ayırdım.
18 Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
İsrail'de ilk doğan erkek çocukların yerine Levililer'i seçtim.
19 Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
İsrailliler kutsal yere yaklaştıklarında belaya uğramamaları için, onların adına Buluşma Çadırı'ndaki hizmeti yerine getirmek ve günahlarını bağışlatmak üzere, onların arasından Levililer'i Harun'la oğullarına armağan olarak verdim.”
20 Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Musa, Harun ve bütün İsrail topluluğu Levililer için söyleneni yaptılar. İsrailliler RAB'bin Musa'ya Levililer'le ilgili verdiği her buyruğu yerine getirdiler.
21 Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
Levililer kendilerini günahtan arındırıp giysilerini yıkadılar. Sonra Harun onları RAB'bin huzurunda adak olarak adadı; onları arındırmak için günahlarını bağışlattı.
22 Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Bundan sonra Levililer Harun'la oğullarının sorumluluğu altında Buluşma Çadırı'ndaki hizmetlerini yapmaya geldiler. RAB'bin Levililer'e ilişkin Musa'ya verdiği buyrukları yerine getirdiler.
23 Bwana akamwambia Mose,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
24 “Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
“Levililer'le ilgili kural şudur: Yirmi beş ve daha yukarı yaşta olanlar Buluşma Çadırı'nda hizmet edecekler.
25 lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
Ancak elli yaşına gelince yaptıkları hizmetten ayrılıp bir daha çadırda çalışmayacaklar.
26 Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”
Buluşma Çadırı'nda görev yapan kardeşlerine yardımcı olacaklar, ama kendileri hizmet etmeyecekler. Levililer'in sorumluluklarını böyle düzenleyeceksin.”