< Hesabu 8 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Potem Pan rzekł do Mojżesza, mówiąc:
2 “Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
Powiedz Aaronowi, a rzecz mu: Gdy zapalisz lampy, siedem lamp przeciwko świecznikowi świecić będą.
3 Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
I uczynił tak Aaron, a przeciwko świecznikowi zapalił lampy jego, jako był rozkazał Pan Mojżeszowi.
4 Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
A była robota świecznika z ciągnionego złota, i słupiec jego, i kwiaty jego ciągnione były; na ten kształt, jaki był Pan ukazał Mojżeszowi, tak urobił świecznik.
5 Bwana akamwambia Mose:
Potem rzekł Pan do Mojżesza, mówiąc:
6 “Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
Weźmij Lewity z pośród synów Izraelskich, a oczyść je.
7 Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
A to uczynisz oczyszczając je: Pokropisz je wodą oczyszczenia; ciż ogolą brzytwą wszystko ciało swoje, a uprawszy szaty swe, czystymi będą.
8 Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Potem wezmą cielca młodego, z ofiarą jego śniedną, mąki pszennej, zagniecionej z oliwą, a cielca młodego drugiego weźmiesz na ofiarę za grzech.
9 Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
I przywiedziesz Lewity przed namiot zgromadzenia, a przyzowiesz wszystkiego zgromadzenia synów Izraelskich;
10 Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
I postawisz Lewity przed Panem, i włożą synowie Izraelscy ręce swe na Lewity;
11 Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
I ofiarować będzie Aaron Lewity na ofiarę przed panem od synów Izraelskich, aby sprawowali posługi Pańskie.
12 “Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
Lewitowie zaś będą kłaść ręce swe na głowy onych cielców, a ofiarować będziesz jednego za grzech, a drugiego na ofiarę całopalenia Panu ku oczyszczeniu Lewitów.
13 Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Potem postawisz Lewity przed Aaronem, i przed syny jego, a ofiarować je będziesz na ofiarę Panu.
14 Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
I odłączysz Lewity z pośród synów Izraelskich, i będą moimi Lewitowie.
15 “Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
A potem przyjdą Lewitowie, aby służyli w namiocie zgromadzenia, gdy oczyścisz i poświęcisz je na ofiarę.
16 Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
Albowiem właśnie oddani są mnie z pośród synów Izraelskich; za każde otwierające żywot, za każde pierworodne z synów Izraelskich obrałem je sobie,
17 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
Gdyż wszyscy pierworodni z synów Izraelskich moi są z ludzi i z bydła: ode dnia, któregom pobił wszystkie pierworodne w ziemi Egipskiej, poświęciłem je sobie.
18 Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
A przyjąłem Lewity miasto wszelkiego pierworodnego z synów Izraelskich.
19 Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
I dałem Lewity darem Aaronowi i synom jego z pośród synów Izraelskich, aby odprawowali służby miasto synów Izraelskich w namiocie zgromadzenia, i oczyszczali syny Izraelskie, aby nie przyszło na syny Izraelskie karanie, gdyby przystępowali synowie Izraelscy do świątnicy.
20 Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Uczynili tedy Mojżesz i Aaron i wszystko zgromadzenie synów Izraelskich z Lewitami wszystko, co rozkazał Pan Mojżeszowi o Lewitach, tak uczynili z nimi synowie Izraelscy.
21 Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
I oczyścili się Lewitowie, a uprali szaty swoje, i ofiarował je Aaron na ofiarę przed Panem, i oczyścił je Aaron, aby byli czystymi.
22 Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Dopiero potem przystąpili Lewitowie ku sprawowaniu urzędu swego w namiocie zgromadzenia przed Aaronem i przed syny jego; jako rozkazał Pan Mojżeszowi o Lewitach, tak im uczynili.
23 Bwana akamwambia Mose,
Rzekł nadto Pan do Mojżesza, mówiąc:
24 “Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
To też Lewitom należy: Od dwudziestego i piątego roku i wyżej każdy przystąpi, aby sprawował urząd przy posłudze namiotu zgromadzenia.
25 lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
A w pięćdziesiąt lat przestanie pracować w urzędzie, i więcej służyć nie będzie.
26 Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”
Ale nadsługować będzie braci swej w namiocie zgromadzenia straż trzymającym, lecz służby samej odprawować nie będzie. Tak sobie postąpisz z Lewitami w urzędziech ich.

< Hesabu 8 >