< Hesabu 8 >

1 Bwana akamwambia Mose,
LEUM GOD El kaskas nu sel Moses ac fahk,
2 “Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
“Fahk nu sel Aaron lah pacl se el filiya lam itkosr fin nien lam uh, elan oakiya tuh in tolak acn meet.”
3 Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Aaron el oru oana, ac oakiya lam uh tuh kalem kac in tolak mutun nien lam uh.
4 Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
Orekla nien lam uh ke gold tuktuki, lucngi na nwe ten, fal nu ke lumah se su LEUM GOD El fahk nu sel Moses.
5 Bwana akamwambia Mose:
LEUM GOD El fahk nu sel Moses,
6 “Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
“Srela mwet Levi uh liki mwet Israel ngia, ac aknasnasyalosla
7 Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
in ouiya se inge: sroksrokunulosyak ke kof in aknasnas, ac sap elos in resaela manolos nufon, ac ohlla nuknuk lalos uh. Na elos ac fah nasnasla.
8 Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Na elos fah eis soko cow mukul fusr, ac lupan flao karyak ke oil in olive ma eneneyuk nu ke mwe kisa wheat; ac kom fah eis soko pac cow mukul nu ke mwe kisa ke ma koluk.
9 Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
Toko kom orani mwet Israel nukewa ac sap mwet Levi in tuyak ye mutun Lohm Nuknuk Mutal, su pa acn nga muta we.
10 Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
Na mwet Israel elos fah filiya paolos fin sifen mwet Levi uh,
11 Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
ac Aaron el fah kisakunma mwet Levi uh nu sik oana sie mwe sang sriyukla sin mwet Israel uh, tuh elos in oru orekma luk.
12 “Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
Na mwet Levi fah filiya paolos fin sifen cow mukul lukwa; soko ac fah mwe kisa ke ma koluk, ac ma soko ngia nu ke mwe kisa firir. Ouiya se inge in orek ke alu in aknasnas lun mwet Levi.
13 Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
“Kisakunma mwet Levi uh oana sie mwe sang sriyukla nu sik, ac sang tuh Aaron ac wen natul in liyalosyang.
14 Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
In lumah se inge kom fah srela mwet Levi uh liki mwet Israel saya, na elos fah ma nutik.
15 “Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
Tukun kom aknasnasyela ac kisakunla mwet Levi uh, elos ac fah fal in orekma in Lohm Nuknuk Mutal.
16 Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
Nga eisalos in aolla wounse mukul nukewa nutin mwet Israel, ac elos ma na nutik.
17 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
Ke nga tuh onela wounse nukewa nutin mwet Egypt uh, nga tuh akmutalye wen se ma matu oemeet in kais sie sou in Israel, ac wounsien kosro nukewa, tuh in ma nutik sifacna.
18 Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
Inge nga eis mwet Levi in aolla wounse nukewa nutin mwet Israel,
19 Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
ac nga sang kunal Aaron ac wen natul elos in liyaung mwet Levi oana sie mwe kite sin mwet Israel, tuh elos fah orekma in Lohm Nuknuk Mutal nu sin mwet Israel, ac in loango mwet Israel liki ongoiya ma ac ku in sonolos elos fin tuku apkuranla nu ke Acn Mutal.”
20 Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Ouinge Moses, Aaron ac mwet Israel nukewa kisakunla mwet Levi, oana ke LEUM GOD El sapkin nu sel Moses.
21 Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
Mwet Levi elos aknasnasyalos sifacna ac ohlla nuknuk lalos, ac Aaron el kisakunulos oana sie mwe kite sriyukla nu sin LEUM GOD. El oayapa oru alu in aknasnas nu selos.
22 Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Mwet Israel akfalye ma nukewa ma LEUM GOD El sapkin nu sel Moses elan oru ke mwet Levi. Ouinge mwet Levi elos fal in oru orekma in Lohm Nuknuk Mutal ye koko lal Aaron ac wen natul.
23 Bwana akamwambia Mose,
LEUM GOD El fahk nu sel Moses,
24 “Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
“Kais sie mwet Levi su yac longoul limekosryak matwa, ac fah oru orekma kunal in Lohm Nuknuk Mutal sik,
25 lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
na el ac mongla liki orekma kunal ke el sun yac lumngaul matwa.
26 Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”
Tukun pacl sacn, el ku in kasru mwet Levi wial in oru orekma kunalos in Lohm Nuknuk Mutal, tusruktu el tia ku in sifacna orekma. Pa inge ma kom ac oakiya nu ke kulansap lun mwet Levi.”

< Hesabu 8 >