< Hesabu 8 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
2 “Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
Parle à Aaron et tu lui diras: Lorsque tu auras placé les sept lampes, que le chandelier soit dressé à la partie australe. Ordonne donc que les lampes regardent contre le nord vis-à-vis de la table des pains de proposition; c’est contre cette partie que leurs le chandelier regarde, qu’elles devront luire.
3 Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Et Aaron le fit, et il posa les lampes sur le chandelier, comme avait ordonné le Seigneur à Moïse.
4 Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
Or voici la façon du chandelier: il était d’or ductile, tant la tige du milieu, que tout ce qui sortait des deux côtés des branches: c’est selon le modèle que montra le Seigneur à Moïse, que Moïse fit le chandelier.
5 Bwana akamwambia Mose:
Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
6 “Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
Prends les Lévites du milieu d’Israël, et tu les purifieras
7 Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
Selon ce rite: Qu’ils soient aspergés d’eau de purification, et qu’ils rasent tous les poils de leur chair. Et lorsqu’ils auront lavé leurs vêtements, et qu’ils seront purifiés,
8 Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Ils prendront un bœuf des troupeaux, avec sa libation, de la fleur de farine arrosée d’huile: et toi, tu prendras un autre bœuf du troupeau pour le péché;
9 Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
Et tu feras approcher les Lévites devant le tabernacle d’alliance, toute la multitude des enfants d’Israël ayant été convoquée.
10 Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
Et lorsque les Lévites seront devant le Seigneur, les enfants d’Israël poseront leurs mains sur eux,
11 Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
Et Aaron offrira les Lévites en la présence du Seigneur, comme un don de la part des enfants d’Israël, afin qu’ils le servent dans son ministère.
12 “Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
Les Lévites aussi poseront leurs mains sur la tête des bœufs, dont tu sacrifieras l’un pour le péché, et l’autre pour l’holocauste du Seigneur, afin que tu pries pour eux.
13 Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Tu présenteras ensuite les Lévites devant Aaron et ses fils, et tu les consacreras après les avoir offerts au Seigneur,
14 Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
Et tu les sépareras du milieu des enfants d’Israël, afin qu’ils soient à moi;
15 “Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
Et après cela ils entreront dans le tabernacle d’alliance, pour qu’ils me servent. Et c’est ainsi que tu les purifieras et les consacreras pour l’oblation du Seigneur, parce qu’ils m’ont été donnés en don par les enfants d’Israël.
16 Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
C’est en place des premiers-nés qui ouvrent un sein quelconque, que je les ai reçus.
17 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
Car ils sont à moi, tous les premiers-nés des enfants d’Israël, tant des hommes que des bêtes. Depuis le jour que j’ai frappé tout premier-né dans la terre d’Egypte, je les ai consacrés pour moi;
18 Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
Et j’ai pris les Lévites au lieu de tous les premiers-nés des enfants d’Israël;
19 Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
Et j’en ai fait don à Aaron et à ses fils, les tirant du milieu du peuple, pour qu’ils me servent au lieu d’Israël dans le tabernacle d’alliance, et qu’ils prient pour eux, afin qu’il n’y ait pas de plaie sur le peuple, s’il osait approcher du sanctuaire.
20 Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Or, Moïse et Aaron et toute la multitude des enfants d’Israël firent touchant les Lévites ce qu’avait ordonné le Seigneur à Moïse:
21 Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
Ils furent donc purifiés, et ils lavèrent leurs vêtements; et Aaron les éleva en la présence du Seigneur, et il pria pour eux,
22 Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Afin que purifiés, ils entrassent dans le tabernacle d’alliance pour leurs fonctions devant Aaron et ses fils. Comme le Seigneur avait ordonné à Moïse touchant les Lévites, ainsi il fut lait.
23 Bwana akamwambia Mose,
Le Seigneur parla encore à Moïse, disant:
24 “Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
Voici la loi des Lévites: Depuis vingt-cinq ans et au-dessus, ils entreront pour servir dans le tabernacle d’alliance.
25 lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
Et lorsqu’ils auront accompli la cinquantième année d’âge, ils cesseront de servir,
26 Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”
Et ils seront les ministres de leurs frères dans le tabernacle d’alliance, pour garder ce qui leur aura été confié; mais les fonctions elles-mêmes, qu’ils ne les fassent point. Tu régleras ainsi pour les Lévites touchant leur garde.

< Hesabu 8 >