< Hesabu 8 >
Yahweh parla à Moïse, en disant:
2 “Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
« Parle à Aaron et tu lui diras: Lorsque tu placeras les lampes sur le chandelier, c’est sur le devant du chandelier que les sept lampes donneront leur lumière. »
3 Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Aaron fit ainsi; il plaça les lampes sur le devant du chandelier, comme Yahweh l’avait ordonné à Moïse.
4 Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
Le chandelier était fait d’or battu; jusqu’à son pied, jusqu’à ses fleurs, il était d’or battu; Moïse l’avait fait selon le modèle que Yahweh lui avait montré.
Yahweh parla à Moïse, en disant:
6 “Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
« Prends les Lévites du milieu des enfants d’Israël et purifie-les.
7 Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
Voici comment tu les purifieras: Fais sur eux une aspersion d’eau expiatoire; qu’ils passent le rasoir sur tout leur corps, qu’ils lavent leurs vêtements, et qu’ils se purifient ainsi.
8 Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Ils prendront ensuite un jeune taureau pour l’holocauste, avec son oblation de fleur de farine pétrie à l’huile; et tu prendras un second jeune taureau pour le sacrifice pour le péché.
9 Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
Tu feras approcher les Lévites devant la tente de réunion, et tu convoqueras toute l’assemblée des enfants d’Israël.
10 Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
Tu feras approcher les Lévites devant Yahweh, et les enfants d’Israël poseront leurs mains sur les Lévites.
11 Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
Aaron offrira les Lévites en offrande balancée devant Yahweh, de la part des enfants d’Israël, afin qu’ils soient pour faire le service de Yahweh.
12 “Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
Les Lévites poseront leurs mains sur la tête des taureaux, et tu offriras l’un en sacrifice pour le péché, l’autre en holocauste à Yahweh, afin de faire l’expiation pour les Lévites.
13 Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Tu feras tenir les Lévites debout devant Aaron et devant ses fils, et tu les offriras en offrande balancée à Yahweh.
14 Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
Tu sépareras les Lévites du milieu des enfants d’Israël, et les Lévites seront à moi;
15 “Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
après quoi les Lévites viendront faire le service dans la tente de réunion. C’est ainsi que tu les purifieras et que tu les offriras en offrande balancée.
16 Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
Car ils me sont entièrement donnés du milieu des enfants d’Israël; je les ai pris pour moi à la place de tout premier-né, ouvrant le sein de sa mère, de tout premier-né des enfants d’Israël.
17 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
Car tout premier-né des enfants d’Israël est à moi, tant des hommes que des animaux; le jour où j’ai frappé tous les premiers-nés dans le pays d’Égypte, je me les suis consacrés.
18 Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
Et j’ai pris les Lévites à la place de tous les premiers-nés des enfants d’Israël;
19 Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
et j’ai donné entièrement les Lévites à Aaron et à ses fils, du milieu des enfants d’Israël, pour faire le service des enfants d’Israël dans la tente de réunion, pour qu’ils fassent l’expiation pour les enfants d’Israël, afin que les enfants d’Israël ne soient frappés d’aucune plaie, quand ils s’approcheront du sanctuaire. »
20 Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Moïse, Aaron et toute l’assemblée des enfants d’Israël firent à l’égard des Lévites tout ce que Yahweh avait ordonné à Moïse touchant les Lévites; ainsi firent à leur égard les enfants d’Israël.
21 Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
Les Lévites se purifièrent et lavèrent leurs vêtements; Aaron les offrit en offrande balancée devant Yahweh, et il fit l’expiation pour eux, afin de les purifier.
22 Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Après quoi, les Lévites vinrent faire leur service dans la tente de réunion, en présence d’Aaron et de ses fils. Selon ce que Yahweh avait ordonné à Moïse touchant les Lévites, ainsi fit-on à leur égard.
23 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
24 “Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
« Voici ce qui concerne les Lévites. A partir de vingt-cinq ans et au-dessus, le Lévite entrera au service de la tente de réunion pour y exercer une fonction.
25 lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
A partir de cinquante ans, il sortira de fonction et ne servira plus;
26 Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”
il aidera ses frères, dans la tente de réunion, à garder ce qui doit être observé; mais il ne fera plus de service. Tu agiras ainsi à l’égard des Lévites au sujet de leurs fonctions. »