< Hesabu 8 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Yahvé parla à Moïse et dit:
2 “Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
Parle à Aaron, et dis-lui: « Quand tu allumeras les lampes, les sept lampes éclaireront devant le chandelier. »
3 Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Aaron fit ainsi. Il en alluma les lampes pour éclairer la zone située devant le chandelier, comme Yahvé l'avait ordonné à Moïse.
4 Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
Voici le travail du chandelier: c'était un travail d'or battu. Depuis sa base jusqu'à ses fleurs, il était travaillé. Il fit le chandelier d'après le modèle que Yahvé avait montré à Moïse.
5 Bwana akamwambia Mose:
Yahvé parla à Moïse et dit:
6 “Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
« Prends les Lévites parmi les enfants d'Israël et purifie-les.
7 Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
Voici ce que tu leur feras pour les purifier: tu les aspergeras d'eau de purification, ils se raseront tout le corps avec un rasoir, ils laveront leurs vêtements et se purifieront.
8 Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Ils prendront ensuite un jeune taureau et son offrande de farine, de la farine fine mélangée à de l'huile, et un autre jeune taureau que tu prendras pour le sacrifice pour le péché.
9 Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
Tu présenteras les Lévites devant la Tente d'assignation. Tu rassembleras toute la congrégation des enfants d'Israël.
10 Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
Tu présenteras les Lévites devant l'Éternel. Les enfants d'Israël imposeront leurs mains sur les Lévites,
11 Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
et Aaron offrira les Lévites devant Yahvé en sacrifice par agitation au nom des enfants d'Israël, afin qu'ils soient au service de Yahvé.
12 “Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
« Les Lévites poseront leurs mains sur la tête des taureaux, et vous offrirez l'un en sacrifice pour le péché et l'autre en holocauste à Yahvé, afin de faire l'expiation pour les Lévites.
13 Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Tu feras passer les Lévites devant Aaron et devant ses fils, et tu les offriras en offrande à l'Éternel.
14 Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
Tu sépareras ainsi les Lévites du milieu des enfants d'Israël, et les Lévites seront à moi.
15 “Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
« Après cela, les Lévites entreront pour faire le service de la Tente de la Rencontre. Tu les purifieras et tu les offriras en sacrifice par agitation.
16 Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
Car ils me sont entièrement donnés d'entre les enfants d'Israël; à la place de tous ceux qui ouvrent le ventre, des premiers-nés de tous les enfants d'Israël, je les ai pris pour moi.
17 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
Car tous les premiers-nés des enfants d'Israël sont à moi, tant les hommes que les animaux. Le jour où j'ai frappé tous les premiers-nés au pays d'Égypte, je les ai sanctifiés pour moi.
18 Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
J'ai pris les Lévites à la place de tous les premiers-nés des enfants d'Israël.
19 Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
J'ai donné les Lévites en cadeau à Aaron et à ses fils parmi les enfants d'Israël, pour qu'ils fassent le service des enfants d'Israël dans la Tente d'assignation et qu'ils fassent l'expiation pour les enfants d'Israël, afin qu'il n'y ait pas de plaie parmi les enfants d'Israël quand ils s'approchent du sanctuaire. »
20 Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Moïse, Aaron et toute l'assemblée des enfants d'Israël firent ainsi aux Lévites. Les enfants d'Israël firent à l'égard des Lévites tout ce que Yahvé avait ordonné à Moïse.
21 Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
Les Lévites se purifièrent du péché et lavèrent leurs vêtements; Aaron les offrit en sacrifice par agitation devant Yahvé et Aaron fit pour eux l'expiation pour les purifier.
22 Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Après cela, les Lévites entrèrent pour faire leur service dans la Tente de la Rencontre, devant Aaron et devant ses fils; ils firent à leur égard ce que l'Éternel avait ordonné à Moïse concernant les Lévites.
23 Bwana akamwambia Mose,
Yahvé parla à Moïse et dit:
24 “Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
« Voici ce qui est assigné aux Lévites: à partir de l'âge de vingt-cinq ans, ils iront faire le service dans l'ouvrage de la Tente de la Rencontre;
25 lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
et à partir de l'âge de cinquante ans, ils se retireront de l'ouvrage et ne feront plus de service,
26 Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”
mais ils assisteront leurs frères dans la Tente de la Rencontre, pour faire le service, et ne feront plus de service. C'est ainsi que tu feras accomplir leurs tâches aux Lévites. »

< Hesabu 8 >