< Hesabu 8 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Jahve reče Mojsiju:
2 “Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
“Govori Aronu i reci mu: 'Kad budeš palio svjetionice, neka sedam svjetionica svijetli na prednjoj strani svijećnjaka.'”
3 Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Aron i učini tako: smjesti svjetionice na prednju stranu svijećnjaka, kako je Jahve Mojsiju naredio.
4 Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
Svijećnjak bijaše skovan od zlata; skovan od svoga podnožja do svoje čaške. Svijećnjak je bio napravljen prema uzorku što ga je Jahve pokazao Mojsiju.
5 Bwana akamwambia Mose:
Jahve reče Mojsiju:
6 “Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
“Uzmi levite između Izraelaca i očisti ih!
7 Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
Ovako s njima postupi da ih očistiš: poškropi ih vodom za okajavanje; a oni neka se obriju po svemu svome tijelu, neka operu svoju odjeću i bit će čisti.
8 Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Neka zatim uzmu jednog junca i prinosnicu od najboljeg brašna, zamiješena u ulju. A ti uzmi drugog junca za okajnicu.
9 Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
Dovedi onda levite pred Šator sastanka i skupi svu izraelsku zajednicu.
10 Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
Kad dovedeš levite pred Jahvu, neka Izraelci stave na njih svoje ruke.
11 Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
Neka zatim Aron prinese levite, kao prikaznicu pred Jahvom, u ime Izraelaca. Tako će njihov posao biti da služe Jahvi.
12 “Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
Neka potom leviti stave svoje ruke juncima na glave; onda jednoga prinesi kao okajnicu, a drugoga kao paljenicu Jahvi, da se izvrši obred pomirenja nad levitima.
13 Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Stavivši levite pred Arona i njegove sinove, prikaži ih Jahvi žrtvom prikaznicom.
14 Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
Odvoji tako levite između Izraelaca da budu moji.
15 “Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
Poslije toga, pošto ih očistiš i prineseš žrtvom prikaznicom, neka leviti uđu u službu Šatora sastanka.
16 Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
Jer oni su između Izraelaca meni potpuno darovani; njih sam sebi uzeo namjesto svih koji otvaraju majčinu utrobu, svih izraelskih prvorođenaca.
17 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
Svako, naime, prvorođenče među Izraelcima, kako čedo tako i živinče, moje je; sebi sam ih posvetio onoga dana kad sam pobio svu prvorođenčad u zemlji egipatskoj.
18 Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
Tako sam uzeo levite namjesto svih izraelskih prvorođenaca.
19 Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
I predao sam levite između Izraelaca kao dar Aronu i njegovim sinovima da mjesto Izraelaca obavljaju službu u Šatoru sastanka; da nad njima obavljaju obred pomirenja, tako da kakva nedaća ne bi pogodila Izraelce što bi se približili Svetištu.”
20 Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Mojsije, Aron i sva izraelska zajednica učine tako s levitima; kako je Jahve naredio Mojsiju za levite, tako im Izraelci i učine.
21 Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
Leviti se očiste i operu svoju odjeću; onda ih Aron prinese pred Jahvu žrtvom prikaznicom. Aron nad njima obavi obred pomirenja da ih očisti.
22 Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Poslije toga uđu leviti u službu u Šator sastanka, u nazočnosti Arona i njegovih sinova. Kako je Jahve naredio Mojsiju za levite, tako su s njima i uradili.
23 Bwana akamwambia Mose,
Jahve reče Mojsiju:
24 “Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
“I ovo se tiče levita: od dvadeset i pet godina naviše neka leviti po redu preuzimaju službu u Šatoru sastanka.
25 lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
A kad kome bude pedeset godina, neka istupi iz službe i neka više ne služi.
26 Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”
Ali može pomagati svojoj braći u vršenju njihovih dužnosti u Šatoru sastanka, no sam ne mora vršiti službe. Tako postupi prema levitima za njihove dužnosti!”

< Hesabu 8 >