< Hesabu 7 >
1 Mose alipomaliza kuisimamisha Maskani, aliitia mafuta na kuiweka wakfu pamoja na samani zake zote. Pia alitia madhabahu mafuta na kuiweka wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
Nowe when Moses had finished the setting vp of the Tabernacle, and anointed it and sanctified it, and all the instruments thereof, and the altar with al the instruments thereof, and had anoynted them and sanctified them,
2 Ndipo viongozi wa Israeli, wale wakuu wa jamaa waliokuwa viongozi wa kabila wasimamizi wa wale waliohesabiwa, wakatoa sadaka.
Then the princes of Israel, heads ouer the houses of their fathers (they were the princes of the tribes, who were ouer them that were nombred) offred,
3 Walizileta kama matoleo yao mbele za Bwana: magari sita ya kukokotwa yaliyofunikwa, pamoja na maksai kumi na wawili; yaani maksai mmoja kutoka kwa kila kiongozi, na gari moja la kukokotwa kutoka kwa kila viongozi wawili. Haya waliyaleta mbele ya Maskani.
And brought their offring before the Lord, sixe couered charets, and twelue oxen: one charet for two princes, and for euery one an oxe, and they offred them before the Tabernacle.
And the Lord spake vnto Moses, saying,
5 “Vikubali vitu hivi kutoka kwao, ili viweze kutumika katika kazi kwenye Hema la Kukutania. Wapatie Walawi kama kazi ya kila mtu itakavyohitaji.”
Take these of them, that they may be to doe the seruice of the Tabernacle of the Congregation, and thou shalt giue them vnto the Leuites, to euery man according vnto his office.
6 Hivyo Mose akachukua yale magari ya kukokotwa pamoja na maksai, na kuwapa Walawi.
So Moses tooke the charets and the oxen, and gaue them vnto the Leuites:
7 Aliwapa Wagershoni magari mawili ya kukokotwa na maksai wanne, kama walivyohitaji kwa kazi yao,
Two charets and foure oxen hee gaue to the sonnes of Gershon, according vnto their office.
8 na pia aliwapa Wamerari magari manne ya kukokotwa na maksai wanane, kama kazi yao ilivyohitaji. Wote walikuwa chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani, Aroni.
And foure charets and eight oxen hee gaue to the sonnes of Merari according vnto their office, vnder the hand of Ithamar the sonne of Aaron the Priest.
9 Lakini Mose hakuwapa Wakohathi chochote kati ya hivyo, kwa sababu walitakiwa kubeba vitu vitakatifu mabegani mwao, vile walikuwa wanawajibika.
But to the sonnes of Kohath he gaue none, because the charge of the Sanctuarie belonged to them, which they did beare vpon their shoulders.
10 Wakati madhabahu yalitiwa mafuta, viongozi walileta sadaka zao kwa ajili ya kule kuwekwa wakfu kwake na kuziweka mbele ya madhabahu.
The princes also offered in the dedication for the altar in the day that it was anoynted: then the princes offered their offering before the altar.
11 Kwa maana Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Kila siku kiongozi mmoja ataleta sadaka yake ili kuwekwa wakfu madhabahu.”
And the Lord sayd vnto Moses, One prince one day, and an other prince an other day shall offer their offring, for the dedication of the altar.
12 Yule ambaye alileta sadaka yake siku ya kwanza alikuwa Nashoni, mwana wa Aminadabu, wa kabila la Yuda.
So then on the first day did Nahshon the sonne of Amminadab of ye tribe of Iudah offer his offring.
13 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
And his offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuenty shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both ful of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
14 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
An incense cup of gold of tenne shekels, ful of incense,
15 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yeere olde for a burnt offring,
16 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
17 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
And for peace offrings, two bullockes, fiue rams, fiue hee goates, and fiue lambes of a yeere olde: this was the offring of Nahshon the sonne of Amminadab.
18 Siku ya pili yake Nethaneli mwana wa Suari, kiongozi wa kabila la Isakari, alileta sadaka yake.
The second day Nethaneel, the sonne of Zuar, prince of the tribe of Issachar did offer:
19 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
Who offred for his offring a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both ful of fine floure, mingled with oyle, for a meat offring,
20 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
An incense cup of gold of ten shekels, ful of incense,
21 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yeere olde for a burnt offring,
22 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
23 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Suari.
And for peace offrings, two bullockes, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yeere olde: this was the offring of Nethaneel the sonne of Zuar.
24 Siku ya tatu Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa kabila la Zabuloni, alileta sadaka yake.
The third day Eliab the sonne of Helon prince of the children of Zebulun offred.
25 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirty shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both ful of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
26 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, ful of incense,
27 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yeere olde for a burnt offring,
28 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
29 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana wa Heloni.
And for peace offrings, two bullockes, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yeere olde: this was the offering of Eliab the sonne of Helon.
30 Siku ya nne Elisuri mwana wa Shedeuri, kiongozi wa kabila la Reubeni, alileta sadaka yake.
The fourth day Elizur ye sonne of Shedeur prince of the children of Reuben offred.
31 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuary, both ful of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
32 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, full of incense,
33 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yere olde for a burnt offring,
34 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
35 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elisuri mwana wa Shedeuri.
And for a peace offring, two bullockes, fiue rammes, fiue hee goates, and fiue lambes of a yere olde: this was the offering of Elizur the sonne of Shedeur.
36 Siku ya tano Shelumieli mwana wa Surishadai, kiongozi wa watu wa Simeoni, alileta sadaka yake.
The fifth day Shelumiel the sonne of Zurishaddai, prince of the children of Simeon offered.
37 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuary, both ful of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
38 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, full of incense,
39 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yeere olde for a burnt offring,
40 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
41 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Shelumieli mwana wa Surishadai.
And for a peace offring, two bullocks, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yere old: this was the offering of Shelumiel the sonne of Zurishaddai.
42 Siku ya sita Eliasafu mwana wa Deueli, kiongozi wa watu wa Gadi, alileta sadaka yake.
The sixt day Eliasaph the sonne of Deuel prince of the children of Gad offred.
43 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both ful of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
44 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, full of incense,
45 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yere olde, for a burnt offring,
46 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
47 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deueli.
And for a peace offering, two bullockes, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yere olde: this was the offring of Eliasaph the sonne of Deuel.
48 Siku ya saba Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa watu wa Efraimu, alileta sadaka yake.
The seuenth day Elishama the sonne of Ammiud prince of the children of Ephraim offered.
49 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuary, both full of fine floure, mingled with oyle, for a meate offering,
50 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, full of incense,
51 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yeere olde for a burnt offring,
52 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
53 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elishama mwana wa Amihudi.
And for a peace offring, two bullockes, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yeere olde: this was the offring of Elishama the sonne of Ammiud.
54 Siku ya nane Gamalieli mwana wa Pedasuri, kiongozi wa watu wa Manase, alileta sadaka yake.
The eight day offred Gamliel the sonne of Pedazur, prince of the children of Manasseh.
55 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both full of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
56 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, full of incense,
57 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yeere olde for a burnt offring,
58 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
59 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Gamalieli mwana wa Pedasuri.
And for a peace offring, two bullockes, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yeere olde: this was the offring of Gamliel the sonne of Pedazur.
60 Siku ya tisa Abidani mwana wa Gideoni, kiongozi wa watu wa Benyamini, alileta sadaka yake.
The ninth day Abidan the sonne of Gideoni prince of the children of Beniamin offered.
61 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both full of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
62 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, full of incense,
63 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yeere olde for a burnt offring,
64 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
65 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gideoni.
And for a peace offring, two bullockes, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yeere olde: this was the offring of Abidan the sonne of Gideoni.
66 Siku ya kumi Ahiezeri mwana wa Amishadai, kiongozi wa watu wa Dani, alileta sadaka yake.
The tenth day Ahiezer the sonne of Ammishaddai, prince of the children of Dan offred.
67 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both full of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
68 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels full of incense,
69 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yeere olde for a burnt offring,
70 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
71 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahiezeri mwana wa Amishadai.
And for a peace offring, two bullocks, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yeere olde: this was the offring of Ahiezer the sonne of Ammishaddai.
72 Siku ya kumi na moja Pagieli mwana wa Okrani, kiongozi wa watu wa Asheri, alileta sadaka yake.
The eleuenth day Pagiel the sonne of Ocran, prince of the children of Asher offred.
73 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both full of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
74 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, ful of incense,
75 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yere olde for a burnt offring,
76 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
77 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
And for a peace offring, two bullockes, fiue rams, fiue he goates, fiue lambes of a yeere olde: this was the offring of Pagiel the sonne of Ocran.
78 Siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa watu wa Naftali, alileta sadaka yake.
The twelfth day Ahira the sonne of Enan, prince of the children of Naphtali offred,
79 Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
His offring was a siluer charger of an hundreth and thirtie shekels weight, a siluer boule of seuentie shekels, after the shekel of the Sanctuarie, both full of fine floure, mingled with oyle, for a meate offring,
80 sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
A golden incense cup of ten shekels, ful of incense,
81 fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
A yong bullocke, a ram, a lambe of a yere olde for a burnt offring,
82 mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
An hee goate for a sinne offring,
83 maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahira mwana wa Enani.
And for peace offerings, two bullockes, fiue rammes, fiue hee goates, fiue lambes of a yeere olde: this was the offering of Ahira the sonne of Enan.
84 Hizi ndizo zilikuwa sadaka za viongozi wa Israeli madhabahu yalipowekwa wakfu, wakati yalitiwa mafuta: sahani kumi na mbili za fedha, bakuli kumi na mbili za fedha za kunyunyizia, na masinia kumi na mawili ya dhahabu.
This was the dedication of the Altar by the princes of Israel, whe it was anointed: twelue chargers of siluer, twelue siluer boules, twelue incense cuppes of golde,
85 Kila sahani ya fedha ilikuwa na uzito wa shekeli 130, na kila bakuli la fedha la kunyunyizia lilikuwa na uzito wa shekeli sabini. Masinia yote kumi na mawili yalikuwa na uzito wa shekeli 2,400kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Euery charger, conteining an hundreth and thirtie shekels of siluer, and euery boule seuentie: all the siluer vessell conteined two thousande and foure hundreth shekels, after the shekell of the Sanctuarie.
86 Sahani kumi na mbili za dhahabu zilizojazwa uvumba zilikuwa na uzito wa shekeli kumi kila moja, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Kwa jumla, sahani za dhahabu zilikuwa na uzito wa shekeli 120.
Twelue incense cups of gold ful of incense, conteining ten shekels euery cup, after the shekell of the Sanctuarie: all the gold of the incense cups was an hundreth and twentie shekels.
87 Jumla ya wanyama waliotolewa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa walikuwa fahali kumi na wawili wachanga, kondoo dume kumi na wawili na wana-kondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja, pamoja na sadaka zao za nafaka. Mbuzi waume kumi na wawili walitolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi.
All the bullockes for the burnt offering were twelue bullocks, the rams twelue, the lambs of a yeere olde twelue, with their meate offrings, and twelue hee goates for a sinne offring.
88 Jumla ya wanyama kwa ajili ya dhabihu ya sadaka ya amani walikuwa maksai ishirini na wanne, kondoo dume sitini, mbuzi dume wa mwaka mmoja sitini na wana-kondoo dume wa mwaka mmoja sitini. Hizi ndizo zilikuwa sadaka zilizoletwa kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu baada ya kutiwa mafuta.
And all the bullocks for the peace offrings were foure and twentie bullockes, the rammes sixtie, the hee goates sixtie, the lambes of a yeere olde sixtie: this was the dedication of the Altar, after that it was anointed.
89 Mose alipoingia kwenye Hema la Kukutania kuzungumza na Bwana, alisikia sauti ikisema naye kutoka kati ya wale makerubi wawili waliokuwa juu ya kile kiti cha rehema, juu ya Sanduku la Ushuhuda. Mose akazungumza naye.
And when Moses went into the Tabernacle of the Congregation, to speake with God, he heard the voyce of one speaking vnto him from the Merciseat, that was vpon the Arke of the Testimonie betweene the two Cherubims, and he spake to him.