< Hesabu 36 >

1 Viongozi wa jamaa ya ukoo wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase, waliokuwa wametoka katika koo za wazao wa Yosefu, walikuja na kuzungumza mbele ya Mose na viongozi, wakuu wa jamaa ya Waisraeli.
The heads of the fathers’ households of the family of the children of Gilead, the son of Machir, the son of Manasseh [Causing to forget], of the families of the sons of Joseph [May he add], came near, and spoke before Moses [Drawn out], and before the princes, the heads of the fathers’ households of the children of Israel [God prevails].
2 Wakasema, “Bwana alipomwamuru bwana wangu kuwapa Waisraeli nchi kama urithi kwa kura, alikuamuru kutoa urithi wa ndugu yetu Selofehadi kwa binti zake.
They said, “Adonai enjoined my lord to give the land for inheritance by lot to the children of Israel [God prevails]. My lord was enjoined by Adonai to give the inheritance of Zelophehad our brother to his daughters.
3 Sasa ikiwa wataolewa na watu wa makabila mengine ya Kiisraeli, itakuwa kwamba urithi wao utaondolewa kutoka urithi wa mababu zetu na kuongezwa katika urithi wa kabila ambalo dada hao wameolewa. Kwa hiyo sehemu ya urithi tuliyogawiwa itachukuliwa kutoka kwetu.
If they are married to any of the sons of the other tribes of the children of Israel [God prevails], then will their inheritance be taken away from the inheritance of our fathers, and will be added to the inheritance of the tribe to which they shall belong. So will it be taken away from the lot of our inheritance.
4 Wakati mwaka wa Yubile kwa Waisraeli utafika, urithi wao utaongezwa kwa lile kabila ambalo wameolewa, na mali yao itaondolewa kutoka urithi wa kabila la mababu zetu.”
When the Jubilee ·Shofar· of the children of Israel [God prevails] shall be, then will their inheritance be added to the inheritance of the tribe to which they shall belong. So their inheritance will be taken away from the inheritance of the tribe of our fathers.”
5 Ndipo kwa agizo la Bwana Mose akatoa amri ifuatayo kwa Waisraeli: “Kile wazao wa kabila la Yosefu wanachosema ni kweli.
Moses [Drawn out] enjoined the children of Israel [God prevails] according to Adonai’s word, saying, “The tribe of the sons of Joseph [May he add] speaks right.
6 Hivi ndivyo Bwana anavyoamuru kwa binti za Selofehadi: Wanaweza kuolewa na mtu yeyote wampendaye, mradi tu waolewe miongoni mwa koo za kabila za baba yao.
This is the thing which Adonai does enjoin concerning the daughters of Zelophehad, saying, ‘Let them be married to whom they think best; only they shall marry into the family of the tribe of their father.
7 Hakuna urithi katika Israeli utakaohamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila jingine, kwa kuwa kila Mwisraeli atatunza ardhi ya kabila lake aliyoirithi kutoka kwa baba zake.
So shall no inheritance of the children of Israel [God prevails] move from tribe to tribe; for the children of Israel [God prevails] shall all keep the inheritance of the tribe of his fathers.
8 Kila binti atakayerithi ardhi katika kabila lolote la Israeli ni lazima aolewe na mtu kutoka kabila na ukoo wa baba yake, ili kila Mwisraeli amiliki urithi wa baba zake.
Every daughter who possesses an inheritance in any tribe of the children of Israel [God prevails] shall be wife to one of the family of the tribe of her father, that the children of Israel [God prevails] may each possess the inheritance of his fathers.
9 Hakuna urithi uwezao kuhamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila jingine, kwa kuwa kila kabila la Israeli litatunza nchi linayorithi.”
So shall no inheritance move from one tribe to another tribe; for the tribes of the children of Israel [God prevails] shall each keep his own inheritance.’”
10 Kwa hiyo binti za Selofehadi wakafanya kama Bwana alivyomwamuru Mose.
The daughters of Zelophehad did as Adonai enjoined Moses [Drawn out]:
11 Binti za Selofehadi, ambao ni Mahla, Tirsa, Hogla, Milka na Noa, wakaolewa na waume, wana wa ndugu za baba yao.
for Mahlah, Tirzah, Hoglah, Milcah, and Noah [Rest], the daughters of Zelophehad, were married to their dod ·father’s· brothers’ sons.
12 Waliolewa ndani ya koo za wazao wa Manase mwana wa Yosefu, na urithi wao ukabaki katika ukoo na kabila la baba yao.
They were married into the families of the sons of Manasseh [Causing to forget] the son of Joseph [May he add]. Their inheritance remained in the tribe of the family of their father.
13 Haya ndiyo maagizo na masharti ambayo Bwana aliwapa Waisraeli kupitia Mose katika tambarare za Moabu, karibu na Yordani ngʼambo ya Yeriko.
These are the mitzvot ·instructions· and the judgments which Adonai enjoined by the hand of Moses [Drawn out] to the children of Israel [God prevails] in the plains of Moab [From father] by the Jordan [Descender] across from Jericho [Fragrant, Moon].

< Hesabu 36 >